Monday, 13 March 2017

KILIMO CHA VIAZI MVIRINGO ..KINAENDELEA..

WADUDU WASUMBUFU WA VIAZI MVIRINGO
1.      Wadudu nondo (Potato tuber month)
Wadudu nondo kitaalam kama (Phthoremaea operculella) hupatikana katika maeneo ya kuhifadhia viazi hasa kwenye maghala na katika mashamba ya viazi. Wadudu hawa athari zake hazionekani kwa urahisi, pia kiazi kilichoshambulia na wadudu hawa, huweza kuota shambani, lakini viazi vilivyoathrika huanza kuoza mara tu vinapovunwa na kuwekwa kwenye
ghala. Wadudu hawa ni hatari sana hasa kwa wakulima wa mbegu za viazi, kwani hupunguza ubora wa mbegu, hali inayopelekea kushuka hata kwa bei ya mbegu hizo, na wakati mwingine kukataliwa na wakaguzi wa mbegu.

DALILI ZA UHARIBIFU
Wadudu nondo huathiri viazi na majani. Mabuu hushambulia sana viazi vikiwa shambani au vikiwa kwenye ghala. Hata hivyo, dalili nyingi za wadudu hawa hutokea kwenye ghala.Kinyesi cha wadudu hawa huweza kuonekana juu ya kiazi cheyewe.  Wadudu hawa pia hushambulia mashina na majani ya viazi.

Jinsi ya kudhibiti wadudu nondo
1.      Kwa kutumia mbegu iliyo safi na isiyokuwa na maginjwa.
2.      Kuteketeza viazi na mimea yote ya viazi iliyoathrika
3.      Kuweka matuta mara tu baada ya kupanda. Hii huzuia wadudu nondo kutaga mayai juu ya viazi, kisha kuzalisha viwavi ambao wataingia ndani ya kiazi na kuzaliana.
4.      Kukata mashina ya viazi siku 90 baada ya kupanda. Hii huzuia mabuu kwenye majani kutoka kuhamia kwenye viazi na kwenye udongo
5.      Kutumia kilimo cha mzunguko wa mazao - Mzunguko wa mimea ni njia nzuri ya kuvunja mzunguko wa uzazi wa wadudu nondo.

Wadudu mafuta (aphid)
Wadudu hawa mara zote hawawezi kukosekana ndani ya shamba la viazi mviringo, wadudu mafuta huanza kushambulia mimea ya viazi tangu kuchipua hadi kukomaa kwa viazi. Mwonekano wao ni wadogo sana, laini na wenye rangi ya kijani-njano. Wakishakuwa wakubwa wadudu hawa huweza kuruka kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine, wakiambukiza na kusambaza magonjwa.

DALILI ZA UHARIBIFU
Mara nyingi wadudu mafuta wanapokuwa kwenye mimea, huwa wanafyonza maji maji yote kwenye mashina na majani tete, hali ambayo husababisha kukauka kwa majni yaliyokwisha kutokeza. Pia huzuia kufunguka kwa majani yanayotokeza kwenye incha.

Wadudu mafuta wenye mabawa huweza kuruka na kueneza magonjwa ya virusi, kwenye mmea mwingine, endapo atakuwa amefyonza virusi kutoka kwenye mmea uliokwisha ambukizwa na magonjwa ya virusi.

Jinsi ya kudhibiti wadudu mafuta
Wadudu mafuta wanaweza kudhibitiwa kwa kupuliziwa madawa ya kuulia wadudu kama Selecron, au Dimethiote. Pia wadudu hawa huwa wanaondolewa shambani kama shamba litakuwa na wadudu wanaoitwa mende wa viazi (Potato corrolado bettle). Mende hao chakula chao kikuu ni wadudu mafuta, hivyo mkulima anaweza kutambua kuwa shamba lake halina wadudu mafuta iwapo shambani kutakuwa na hawa mende wa viazi. Pia mkulima iwapo hatawadibiti hawa mende wa viazi, wakimaliza kula wadudu mafuta, mwishowe huanza kutoboa majani ya viazi, kisha na kusababisha kukauka kwa kwa mmea.

Wadudu chiriku (Thrips)
Wadudu hawa ni wadogo sana kwa umbo, wenye tumbo refu na huwa wenye rangi ya manjano na wangine wana rangi nyeusi.
Wadudu hawa mar azote hupatikana kwenye mimea ya viazi tangu ikiwa kama machipukizi mpaka kukomaa kwa viazi.

DALILI ZA UHARIBIFU
Kama ilivyo kwa wadudu mafuta, wadudu chiriku pia kusababisha uharibifu kwa mimea ya viazi.
Wadudu hawa huaribu sehemu ya chini ya majani, kisha hufyonza majimaji yote haliyopo kwenye majani mapya na yaliyo laini, hali ambayo husababisha kukauka kwa mimea.

Vile vile wadudu chiriku wanaweza kubeba na kuenea magonjwa ya virusi kwenye shamba la viazi.

Jinsi ya kudhibiti wadudu chiriku
Wadudu hawa wanaweza kudhibitiwa kwa kufanya haya yafuatayo:
• Kwa kupulizia madawa ya kuulia wadudu
• Kilimo cha mzunguko wa mazao

Viwavi au (cutworm)
Wadudu hawa mara nyingi hupatikana ndani ya udongo, na kuwepo kwa wadudu hao, wanaweza kuanza kukata mashina ya mimea tangu inapochipua mpaka kuvuna. Viwavi kuharibu si tu mimea ya viazi mviringo, pia kuathiri karibu kila aina ya mimea ikiwa ni pamoja magugu.

DALILI ZA UHARIBIFU
Wadudu hawa huharibu mashina ya mimea na mizizi. Dalili huoneka na kwenye mimea baada ya kuona baadhi ya mashina yamekatwa mara tu bada ya kuchipua. Wadudu hawa wanaweza kusababisha hasara kubwa shambani; hasa wakati mimeaina siku 25-35 tangu kupandwa kwa viazi.

Jinsi ya kudhibiti wadudu viwavi
Ili mkulima kuweza kudhibiti wadudu hawa, yafaa kufanya haya yafuatayo;-
1.      Kuondoa na kutaketeza mabuu yote yanaoonekana shambani hasa wakati wa kuandaa shamba na wakati wa kuwekea matuta.
2.      Kupulizia madawa ya kuulia wadudu shambani kabla ya kupanda.


Inzi weupe (whitefly)
Nzi weupe huathiri si tu viazi mviringo bali hata na mazao mengine ya mboga na nafaka.

DALILI ZA UHARIBIFU
Nzi weupe huathiri mimea ya viazi kwa kufyonza majimaji kwenye majani machanga. Majani yaliyoathirika huwa dhaifu na hatimaye kukauka.

Jinsi ya kudhibiti inzi weupe
Inzi weupe huweza kudhibitiwa kwa kupulizia dawa ya kuulia wadudu kama ilivyokwisha tajwa hapo mwanzo.

Matumizi ya viuatilifu vya wadudu
Utangulizi:
Kiuatilifu kwa kawaida siyo dawa bali ni sumu ambayo inaweza kuua aina yoyote ya viumbe hai. Viuatilifu ni kwa ajili ya kuulia wadudu, na vinatumika sana pasipo kufuata maelekezo.  Kwa wakulima wa viazi hasa kipindi cha mvua wanaweza kupulizia dawa hata mara mbili kwa siku. Pia wakulima walio wengi huchanganya aina mbalimbali za viuatilifu wakati wa kutumia shambani.
Kwa ujumla mkulima akichanganya aina mbali mbali za viuatilifu, hupunguza ufanisi wa kiuatilifu, n ahata hivyo kwa kufanya hivyo, huongeza gharama za uzalishaji wa viazi.

AINA ZA VIUATILIFU
 Viuatilifu vya kemikali vinaweza kuwekwa katika makundi mbali mbali kutokana na lengo la matumizi kwa mkulima.

• Kiuatilifu cha kuua wadudu (Insectcides).
• Kiuatilifu kwa ajili ya kuua magugu (Herbicides)
• Kiuatilifu chaye lengo la kutokomeza fangasi (Fungicides).
• Kiuatilifu cheye lengo la kutokomeza minyoo fundo (Nematicides)

VIUATILIFU KULINGANA NA UTENDAJI KAZI WAKE
• Kiuatilifu kinachongandia (Contact pesticides)
Kiuatilifu hiki hufanya kazi kwa kugusana na sehemu yenye ugonjwa. Dawa hizi hubaki kwenye mimea tu baada ya kupulizwa, lakini ni bora na huyafa kazi kwa muda mfupi.

• Kiuatilifu cheye kupenyeza (systemic pesticide)
Hii ni dawa ambayo inaweza kuingia na kupenyeza ndani yam mea na kusambaa sehemu zote za mmea wa kiazi. Kiuatilifu hiki ni kizuri kwani kinatibu na kukinga wadudu pamoja na magonjwa husika. Sumu ya dawa hii hukaa kwa muda mrefu ndani ya mmea. Kiuatilifu hiki hakiruhusiwi kutumika kwenye viazi vilivyo karibu kuvunwa, kwani sumu hukaaa kwa muda mrefu, hivyo kusababisha athari kwa watakaotumia.

JINSI YA KUTUMIA VIUATILIFU MBALIMBALI
Ili kuwa na ufanisi wa dawa za kuzuia na kuua wadudu, hutegemea sana na jinsi mkulima anavyoitumia. Lini na wakati gani dawa itumike ni vitu vya kuzingatia.  Ili kiuatilifu kiweze kufanya kazi vema, yafuatayo lazima yazingatiwe;-

1.      Kiuatilifu kilengwa: Kwa mfano, ili kudhibiti wadudu mafuta, lazima dawa ya kuiua wadudu hao itumike.  Kwa kawaida orodha ya viumbe hai husika huonekana juu ya maandiko ya kifungashio.
2.      Majira sahihi: Majira lazima ni kitu cha msingi kutokana na tabia ya wadudu walengwa na hali ya hewa wakati wa kupiga dawa. Kama wadudu wanaonekana wakati wa asubuhi, ni bora kupiga dawa wakati wa asubuhi pia. Hali ya hewa, hasa mvua na jua, vinaweza kuwa na ushawishi mkubwa sana kwenye utendaji wa kazi ya kiuatilifu.
3.      Kiasi sahihi: kwa kawaida kila kiuatilifu huwa kinamaelezo ya kiasi cha kutumia. Maelezo hayo huwekwa juu ya kifungashio. Hayo maelezo ni lazima kuzingatiwa na mkulim. Mkulima asipo fuata maelekezo ya dawa, basi husababisha dawa isiweze kufanya kazi vizuri, na hutengeneza sugu au ukizani dhini ya ugonjwa au wadudu husika.

4.      Kuchangaya: Viuatilifu havipaswi kuchanganywa wakati wa kutumia, kwani huchangia kupunguza uwezo wa dawa katika kufanya kazi. Na kutengeneza sumu mbaya, inayoweza kuua hata na viumbe visivyolegwa.

Hatari za viuatilifu kwa binadamu na mazingira
Hatari ya madawa ya kuulia wadudu kwa binadamu na mazingira ni:
• Sumu kwa binadamu: Wakulima hutumia madawa ya kuulia wadudu na magonjwa bila ya kuwa na kinga. Husababisha kifo, lakini inaweza kusababisha pia magonjwa ya ngozi kama kansa, kichefuchefu, udhaifu mwilini, maumivu ya kichwa, degedege.
• Kuua viumbe wengine.
• Maji na uchafuzi wa hewa.

MAGONJWA YA VIAZI YASABABISHWAYO NA BAKTERIA

Utangulizi

     Magonjwa ya viazi ni mengi na yameenea sehemu mbalimbali.

    Magonjwa ya viazi hupunguza ubora na wingi wa mazao.

   Magonjwa makuu ya viazi yanayosababishwa na vimelea vya bakteria ni:-

-      Bakteria mnyauko (Bacterial Wilt)

-       Kuoza viazi   (Bacterial soft rot)

Utangulizi

-       Shina jeusi (Blackleg)

-       na Skabi ya kawaida ( Common scabies)

Dalili za Bakteria Mnyauko

    Dalili za mwanzo ni kunyauka kwa majani kuelekea juu.

    Mimea huanza kwa kupooza mchana na jioni hurudia hali yake, mwishowe hupooza kabisa na kufa.

Picha zinaonyesha dalili za ugonjwa wa bakteria mnyauko kwenye mimea ya viazi na nyanya. Pia hushambulia tumbaku, pilipili, mnavu nk.

     Dalili ya pili inayoonekana ni udongo kushika kwenye kiazi baada ya ute wa bakteria kutoka kwenye macho ya kiazi na kukauka.

Kusambaa kwa Bakteria mnyauko

     Maji ya mvua.

    Udongo wenye bakteria unaposogezwa wakati wa kulima au kupalia mazao.

    Udongo wenye vimelea hao ulioshika kwenye vifaa vya shamba km. jembe halo nk.

    Udongo wenye vimelea ulioshika kwenye viatu au buti za shamba

   Magugu ya familia moja na viazi kuhifadhi vimelea vya ugonjwa.

    Kupanda viazi vyenye vimelea bila kuonyesha dalili za ugonjwa.

 

      Kudhibiti Ugonjwa

   Tumia mbegu iliyothibitishwa toka chanzo rasmi.

   Tumia kilimo mzunguko.

   Dhibiti magugu.

 

Shina jeusi (Blackleg)

 

Utangulizi

   Huenezwa kwa kupanda kiazi chenye vimelea.

   Huanza kwa shina kuwa jeusi na majani kunyauka

   Ugonjwa huu haujaenea sana hapa kwetu.

Kuudhiti

    Tumia mimea iliyokuzwa maabara (TC) kuanzisha vizazi vya msingi.

    Panda au zalisha mbegu kwa vizazi vichache. (4)

    Wakati wakuvuna punguza uwezekano wa mikwaruzo na vidonda kwenye kiazi.

   Wakati wa kuhifadhi – mahali pakavu, ubaridi, na mzunguko wa hewa wa kutosha.

Skabi ya kawaida  (Common scabies)

    Ni ugonjwa wa ngozi ya kiazi.

    Hauathiri kiasi cha mazao bali ubora wake.

    Unapunguza muda wa kiazi kuhifadhiwa  na kuongeza kasi viazi kuoza.

    Hushamili ikiwa hali ya udongo ni kavu.

   Unasambazwa na mbegu ya viazi.

Pia hushamili kwenye udongo wenye uchachu chini ya 5.

Kudhibiti

   Kupanda mbegu iliyothibitishwa ubora.

   Panda jamii ya viazi  zenye ukinzani.

   Kuwa makini tunapotumia mbolea zinazoongeza uchachu wa udongo.

   Mwagilia shamba la viazi kwa mpango mzuri.


  Kuoza viazi ni ugonjwa usabishwao na aina tofauti tofauti katika kundi la Pectobacteria.

    Ni ugonjwa wa viazi ghalani (store).

   Kuudhibiti:-

- Safisha na kupulizia dawa sakafu ya ghala kabla ya kuweka viazi.

- Wakati wa kuvuna punguza mikwaruzo na vidonda.

-      Hifadhi viazi vikiwa vimekauka


-      Hakikisha ghala ni safi, lina ubaridi na mzunguko wa hewa wa kutosha.

No comments:

Post a Comment