Wednesday, 1 March 2017

UFUGAJI WA KUKU.

UTANGULIZI

Tanzania ina idadi ya kuku wa kienyeji wanaokadiriwa kuwa million 34 ambao wanafugwa kwa mtindo wa huria. Ufugaji wa aina hii hufanyika vijijini na mijini pia.
Idadi hii ya kuku bado ni ndogo ikilinganishwa na mahitaji halisi ya Watanzania wanaokadiriwa kuwa milioni 45 Ulaji wa nyama ya kuku nchini unakadiriwa kuwa ni wastani wa kilo 0.7 kwa kila mtu kwa mwaka mzima ilihali Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) linakadiria wastani mzuri wa ulaji wa nyama kuwa ni kilo 6.8 kwa mtu kwa mwaka. Hii inaashiria kuwa soko la kuku nchini ni kubwa, ambayo ni fursa muhimu kwa wafugaji wa kuku.
Ufugaji wa kuku ni nyenzo nzuri ya kujipatia kipato katika kaya kwa sababu ufugaji wa kuku hauhitaji mtaji mkubwa na hauna kazi kubwa kiuendeshaji. Katika ufugaji huria,kuku hujitafutia chakula wenyewe. Pia inapowezekana hupewa mabaki ya chakula, chenga, pumba au nafaka yoyote inayopatikana katika mazingira husika. Kwa walio wengi ifikapo nyakati za jioni, kuku hulala jikoni au ndani nyumbani kwa mfugaji mwenyewe. Ufugaji huu ni rahisi kwa kuwa hauna gharama kubwa ila faida yake ni kitoweo tu au fedha kidogo sana.
Kutokana na lishe duni na kuzaana wenyewe kwa wenyewe (bila kubadili jogoo), kuku wa kienyeji walio wengi wana uzito mdogo. Wana wastani wa uzito wa robo tatu za kilo hadi kilo moja wakiwa na umri wa zaidi ya mwaka mmoja. Ila wakitunzwa vizuri zaidi na kuboreshwa wana uwezo wa kufikia uzito wa kilo moja hadi moja na nusu katika umri wa miezi sita hadi nane.
Kwa upande wa utagaji wa mayai kuku wa kienyeji kwa wastani hutaga mayai 50 hadi 65 kwa mwaka. Wakitunzwa vizuri zaidi huweza kufikia uzalishaji wa  mayai 80 hadi 100 kwa mwaka.
Kijitabu hiki kinatoa maelezo ya njia na kanuni mbalimbali rahisi za kuzingatia ili  mfugaji aweze kuzitumia kupata mazao mengi na bora zaidi yatakayomnufaisha kimapato na kwa matumizi mengine.

Kanuni hizi ni pamoja na:

v   Kuchagua njia bora ya kufuga na sifa za mabanda bora ya kuku
v   Kuchagua aina bora ya kuku wa kufuga, kuzaliana na kutotolesha
v   Utunzaji wa vifaranga.
v   Kutengeneza chakula bora cha kuku
v   Kudhibiti na kutibu magonjwa
v   Kutunza kumbukumbu
v   Kutafuta masoko

NJIA TOFAUTI ZA KUFUGA KUKU.

Mambo yanayomfanya mfugaji kuamua atumie njia fulani ya kufuga ni pamoja na uwezo wa  kugharamia shughuli ya ufugaji wa kuku na ukubwa wa eneo alilonalo la kufugia. Katika sehemu hii utajifunza njia tatu za kufuga kuku ambazo ni:
1.                   Kufuga huria.
Kuku huachwa wenyewe kujitafutia chakula na maji. Njia hii inatumika zaidi kufuga kuku wa kienyeji. Mara chache sana mfugaji huwapatia kuku chakula cha ziada. Kwa ufugaji huu lazima kuwe na eneo kubwa la kutosha kuku kuzunguka na kutafuta chakula. Kuku hulala eneo lisilo rasmi
kama vile jikoni, kwenye kiambata n.k.

Faida zake
 Ni njia rahisi ya kufuga.
 Gharama yake pia ni ndogo.
 Kuku wanapata mazoezi ya kutosha.
 Kuku wanapata chakula mchanganyiko ambacho kinafaa kiafya.
 Hasara zake
 Kuku huwa hatarini kuibiwa au kudhurika na wanyama wakali na hali mbaya ya hewa.
 Ukuaji wa kuku ni hafifu, hufikia uzito wa kilo 1.2, baada ya mwaka.
 Huharibu mazingira kama kula na mimea ya bustanini mazao kama nafaka.
 Ni rahisi kuambukizwa magonjwa.
2.                  Kufuga nusu ndani – nusu nje
Huu ni mtindo wa kufuga ambapo kuku wanakuwa na banda lililounganishwana uzio kwa upande wa mbele. Hapa kuku wanaweza kushinda ndani
Wakati wa mchana kuku huwa huru kushinda ndani ya banda hasa wanapotaka kutaga na wakati wa kuatamia au wanaweza kukaa ndani ya uzio nje.

Faida za kufuga nusu ndani na nusu nje

 Kuku wanakuwa salama mbali na maadui mbali mbali.
 Utaweza kuwalisha kuku wako vizuri hivyo wataweza kuongeza uzalishaji wa mayai na wa nyama (kwa kukua haraka).
 Itakuwa rahisi kwako kudhibiti wadudu na vimelea vinavyoweza kuleta magonjwa kwa kuku wako.
 Ni rahisi kuwatenganisha kuku katika makundi tofauti na kuwahudumia ipasavyo.
 Ni rahisi kutambua kuku wagonjwa kuliko kufuga huria.
 Kuku watapata mwanga wa jua wa kutosha pamoja na hewa safi.Wakati wa jua kali watakuwa huru kuingia ndani ya banda na kukaa kivulini.
 Kuku hawatafanya huharibifu wa mazao yako shambani au bustanini na kwa majirani zako.
 Utapata urahisi wa kukusanya na kupeleka mbolea bustanini au shambani.
 Changamoto ya kufuga nusu ndani na nusu nje
 Huna budi uwe na muda wa kutosha kwa ajili ya kuwahudumia kuku wako.
 Pia utahitaji kuwa na eneo kubwa kiasi la kufugia.
 Pia utaingia gharama ya ziada kidogo ya kutengeneza banda na wigo na kuwapatia uku chakula cha ziada.
 Hata hivyo gharama za muda huo na za vifaa vingine zita?diwa na mapato ya ziada utakayopata kwa kufuga kwa njia hii.
3.                   Kufuga ndani ya Banda tu
Njia nyingine ni kuwafuga kuku ndani tu. Katika njia hii, kuku hukaa ndani wakati wote. Njia hii ya ufugaji utumiwa zaidi na wafugaji wa kuku wa kisasa. Lakini yaweza kutumika hata kwa kuku wa asili hasa katika sehemu zenye ufinyu wa maeneo.
Changamoto za ufugaji wa ndani ya banda tu
 Unatakiwa uwe na muda wa kutosha wa kuwahudumia kuku wako kikamilifu.
 Pia unatakiwa kuwa na mtaji mkubwa wa kujenga banda na kuwanunulia kuku chakula.
 Ugonjwa ukiingia na rahisi kuambukizana.Vilevile kuku huweza kuanza tabia mbaya kama kudonoana, n.k.

Faida za kufuga ndani tu
 Ni rahisi kutambua na kudhibiti magonjwa.
 Ni rahisi kudhibiti upotevu wa kuku, mayai na vifaranga.
 Ni rahisi kuwapatia chakula kulingana na mahitaji ya kila kundi.
 Ni rahisi kuwatambua na kuwaondoa kuku wasiozalisha katika kundi.
Ni ufugaji upi unafaa zaidi kutumika kwenye mazingira ya vijijini?     
Kwa ujumla, njia rahisi na inayopendekezwa kutumiwa na mfugaji wa kawaida kijijini ni ya ufugaji wa nusu ndani na nusu nje, yaani nusu huria. Hii inatokana na faida zake kama zilizoainishwa hapo awali. Kwa kutumia mfumo huu wa ufugaji, utaepuka hasara za kufuga kwa mtindo wa huria kama zilivyainishwa mwanzoni mwa sehemu hii ya kitabu hiki.
Pia ukitumia mtindo wa ufugaji wa nusu huria utafanya ufugaji wako kwa njia bora zaidi ndani ya uwezo ulionao, kwa sababu kwa sehemu kubwa utatumia mali ghafi inayopatikana katika eneo lako.

KANUNI ZA UFUGAJI BORA WA KUKU

Watu wengi hapa nchini hujihusisha na ufugaji wa kuku kwa lengo la kujipatia chakula na kipato. Mazao yatokanayo na ufugaji wa kuku ni pamoja na mayai, nyama, mbolea na manyoya kwa matumizi mbalimbali. Mifumo ya ufugaji kuku ambayo hutumika hapa nchini ni huria, nusu huria na shadidi. Ufugaji wa kuku utakuwa endelevu na wenye tija kwa kufuata kanuni za ufugaji bora zifuatazo:-
*             Kufuga kuku  kwenye banda bora,
*             Kuchagua kuku bora wa kufuga,
*             Kutunza na kulisha kuku kulingana na hatua mbalimbali za ukuaji
*             Kudhibiti na kutibu magonjwa ya kuku 
*             Kutunza kumbukumbu.

1  Banda la Kuku
Kuku huhitaji banda bora ili wasiathirike na madhara mbalimbali. Banda bora la kuku linatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:-
ü  Imara, lenye uwezo wa kuwahifadhi kiafya na pia dhidi ya hali ya hewa hatarishi kwa mfano jua kali, upepo, baridi na mvua pamoja na wanyama hatari,
ü  Lenye mwanga, hewa na nafasi ya kutosha inayoruhusu usafi  kufanyika kwa urahisi,
ü  Lijengwe sehemu yenye mwinuko isiyotuama maji, isiyo na upepo mkali na iwe mbali kidogo na nyumba ya kuishi watu,
ü  Liwe na vichanja kwa ajili ya kuku kupumzika na kulala 

ü  Liwe na sehemu ya kuwekea chakula, maji, kutagia, kuatamia na sehemu ya kulelea  vifaranga,
ü  Liwe  na nafasi ya kutosha kulingana na idadi ya kuku na kuweka  vyombo vya chakula na maji,
ü  Kwenye mazingira ya joto banda liwe la  ukuta mfupi na sehemu ya  kubwa  wazi yenye wavu hadi kufikia kwenye paa
ü  Kwenye mazingira ya baridi banda liwe na ukuta mrefu unaokaribia paa na sehemu ndogo tu iwe wazi yenye wavu ili kupitishia hewa na mwanga.

1.1 Vifaa Vinavyotumika kwa Ujenzi wa Banda
Vifaa vya kujengea banda vizingatie gharama na upatikanaji wake katika eneo husika. Baadhi ya vifaa hivyo ni kama ifuatavyo:-
v   Sakafu  -  Saruji, udongo, mbao, mianzi au fito
v   Kuta -  Fito, mabanzi, mbao, nguzo mianzi, udongo, matofali, mawe, mabati na wavu
v   Paa      -   Nyasi, makuti, majani ya migomba, mabati na vigae.
v   Wigo - Matofali, mbao, fito nguzo, mabanzi,  mianzi,matete, wavu na mabati
Vyombo vya Maji   


Kuna njia nyingi za kutengeneza vyombo vya kuwekea maji ya
kuku ya kunywa.
 Aina ya mojawapo unayoweza  kutumia ndoo au debe la lita kumi au ishirini ya plastiki. Kata ndoo hiyo pande nne


kutoa nafasi ya kuku ya kunywea kama kielelezo




kinavyoonyesha. Tengeneza idadi ya vyombo hivi inayowiana na wingi wa kuku ulionao.
 Au waweza kutumia sufuria au beseni pana kiasi. Hii huwekewa tofali au jiwe sa? pana baada ya kuwekewa maji ya kunywa ili kuzuia kuku wadogo wasizame na maji yasichafi liwe kirahisi.
 Vifaa maalum vya kunyweshea kuku vinapatikana katika maduka ya pembejeo za kilimo.
Vyombo vya Chakula
Vyombo hivi ni muhimu viwe vimetengenezwa vizuri ili visiwe chanzo cha upoteaji wa chakula. Unapotengeneza kilishio cha kuku kumbuka kuwa kuku wana tabia ya kuchakura. Husambaza au kupekua chakula kwa miguu hata kwa midomo
ili kupata chakula cha chini.
Tabia hii husababisha kumwagwa kwa chakula kingi chini na kusababisha hasara. Unaweza kudhibiti tatizo hili kwa kutengeneza vyombo visivyoruhusu kuku kuchakura kama inavyoonyeshwa kwenye kielelezo hapa chini.
Unaweza kutengeneza kilishio hiki wewe mwenyewe au fundi seremala waliopo katika eneo unaloishi. Inafaa kilishio kiwe chembamba ili kuku wasiweze kuingia. Pia kinatakiwa kiwe kirefu ili kuku waweze kula bila kusongamana.
Viota
Zipo aina tofauti za viota ambazo hutumika kwa ajili ya kutagia. Ipo aina ya ambayo ni ya kutagia kuku mmoja mmoja. Vipimo vinavyopendekezwa kwa kila kiota ni upana wa sentimita 30, urefu sentimita 30 na kina sentimita 35. Upande wa mbele uachwe wazi
ila sentimita 10 za kwanza kutoka chini zizibwe na ubao Weka idadi ya viota inayotoshelezakuku ulio nao.
Pia ipo aina nyingine inayoweza kutumiwa na kuku zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Ni kama kiota kimoja kilichogawanywa katika vyumba kadhaa. Ila kila chumba kina vipimo kama vya kiota kimoja (angalia picha hapa chini).Aina hii ya kiota ina upanawa sentimita 30 na kina sentimeta 35na urefuwake unategemea idadim ya viota.


Viota vinatakiwa kuwa na giza ili kuku wasiogope kuingia kutaga ndani yake. Pia giza husaidia kupunguza tabia ya kuku kula mayai na kudonoana. Kiota kinafaa kuwekwa mahali ambako ni rahisi kuku kuingia na kutoka. Vile vile iwe ni sehemu itakayorahisisha usafishaji wa kiota chenyewe.
Vichanja
Kuku wana asili ya kupenda kulala au kupumzika sehemu iliyoinuka. Hivyo ndani ya banda weka vichanja vitakavyotosheleza idadi ya kuku waliopo.
UCHAGUZI WA KUKU BORA.
  Kuku wa Asili
Aina za kuku wa asili wanaopatikana hapa nchini ni pamaja na Kuchi (Kuza), pori  (Kishingo), Njachama, Kinyavu, Mbuni na Tongwe (Msumbiji). Mfugaji anaweza kuongeza uzalishaji kwa kuchagua kuku mwenye sifa zifuatazo:-
ü  Uwezo wa kutaga  mayai mengi (kati ya 15-200 katika mzunguko mmoja wa utagaji
ü  Uwezo wa kuatamia na kuangua vifaranga wengi,
ü  Uwezo wa kustahimili  magonjwa
ü  Umbo kubwa na kukua haraka.
Masuala ya Kuzingatia Wakati wa Kumchagua Kuku Mtagaji Asili.
Viungo vya mwili Sifa:
v  Macho Maangavu, yenye wekundu kwa mbali na makubwa yamejaa kwenye soketi za macho. 
v  Mdomo Wenye rangi ya njano kwa mbali
v  Kisunzu/Upanga  Chekundu, Laini,kimelala kidogo upande na kinang’aa Shingo  Iliyosimama ,
v  Umbali kati ya kidali na nyonga , Upanga wa vidole 3-4 vya mpimaji,
v  Upanga wa nyonga Upana wa vidole 3 vya mpimaji.



Kuku wa Kisasa
Kuku bora wa kisasa kwa ajili ya mayai au nyama ni mwenye sifa zifuatazo:-
Ø   Uwezo wa kuanza kutaga  wakiwa na umri mdogo (miezi 5-6) kutegemea na koo,
Ø  Umbo  kubwa na anayekula haraka (kilo 1.5-2.0 kwa kipindi cha wiki 8-120 kutegemea na koo kwa kuku wa nyama,
Ø  Anayetaga mayai mengi (250 au zaidi) kwa kuku wa mayai kwa mwaka; na
Ø  Awe na uwezo wa kutaga katika umri wa miezi 6-8.

  Uchaguzi wa Jogoo Bora wa Mbegu
      Jogoo wa mbegu anatakiwa awe na sifa zifuatazo:-
Ø  Achaguliwe kutoka kwenye koo zenye sifa ya kutaga mayai mengi,
Ø  Mrefu, umbo kubwa, miguu imara na yenye nguvu,
Ø  Awe machachari, ushawishi kwa mitetea na ari ya kupanda
Ø  Uwezo wa kupanda akiwa na umri wa miezi 7-10.

   Uchaguzi wa Mayai kwa ajili ya Kutotoa Vifaranga.

 Mayai kwa ajili ya kutotoa vifaranga yawe na sifa zifuatazo:-
Ø  Yaliyorutubishwa na jogoo,
Ø  Yasiwe na nyufa,
Ø  Yasiwe na maganda tepetepe,
Ø  Yasiwe na kiini kilichovunjika,
Ø  Yawe na ukubwa wa wastani; na
Ø  Yasiwe yamekaa zaidi ya wiki 2 baada ya kutagwa.


Utunzaji wa Mayai
Mayai ya kienyeji kwa ajili ya kutotoa vifaranga yatunzwe kwa kusimamishwa wima sehemu iliyochongoka ikiwa imeangalia chini kwa siku 3 za mwanzo na kisha yageuzwe ili sehemu iliyobutu iangalie chini. Mayai yahifadhiwe kwenye sehemu iliyo na ubaridi kidogo na giza.
Utunzaji wa Kuku kwa Makundi
Utunzaji wa Vifaranga.
Malezi bora ya vifaranga ni muhimu katika ufugaji wa kuku kwa sababu  vifaranga hawana uwezo wa kustahimili mazingira wakiwa wenyewe mara wanapoanguliwa.Ukosefu wa malezi bora  husababisha vifaranga kuwa dhaifu,kufa kwa wingi na hivyo kupunguza idadi ya kuku wa baadaye. Malezi ya vifaranga yanaweza kufanyika kwa kutumia kuku walezi au kutumia vifaa maalum.

Kulea Vifaranga kwa Kutumia Kuku Mlezi
Vifaranga wanaweza kulelewa na mama yao au kuku mlezi. Endapo kuku wengi wametotoa vifaranga kwa wakati mmoja, achaguliwe kuku mlezi aliye na uwezo wa kulea vifaranga wengi  kati ya waliototoa aendelee kulea na wengine waliototoa waachwe huru ili warudi kwenye mzunguko wa kutaga. Kuku mmoja anaweza kulea vifaranga 20 hadi 25. Mfugaji wa kuku,pamoja na kanuni nyingine, anapaswa kuzingatia yafuatayo:-
Ø  Kuku anayelea vifaranga atengewe chumba maalumu, apewe maji ya kutosha na chakula chenye virutubisho muhimu,
Ø  Vifaranga wasiachiwe kutoka nje hadi watakapofika umri wa wiki 6,
Ø  Vifaranga watengwe na mama/mlezi baada ya wiki 4 kuruhusu mama aendelee na mzunguko wa kutaga;na
Ø  Katika maeneo yenye hali ya hewa ya ubaridi vifaranga  wacheleweshwe  kutenganishwa na mama/mlezi hadi wiki ya 6 au mpaka  waonekane  wameota  manyoya  ya  kutosha.


 Kulea Vifaranga kwa  Kutumia Bruda    
Bruda ni chombo/sehemu iliyoandaliwa mahusus kwa ajili ya kuwapatia joto vifaranga badala ya mama/mlezi. Mfugaji anaweza kulea vifaranga wengi kwa kutumia bruda ambayo ni mduara unaweza kutengenezwa kwa kutumia mbao, karatasi ngumu au kwa kuziba pembe za chumba.Aidha, njia hii hupunguza vifo vya vifaranga vinavyosababishwa na ndege au wanyama hatari,huruhusu kuku kutaga mapema zaidi na kuwa na mizunguko mingi ya utagaji (kwa kuku wanaoatamia). Vilevile, hurahisisha udhibiti wa magonjwa.
Mfugaji anapaswa kufuata taratibu zifuatazo katika kulea vifaranga kwa kutumia bruda:-
v  Kuweka vifaa vya kuongeza joto kwa mfano taa ya umeme, chemli au jiko la mkaa. Zingatia kiwango cha joto kinachohitajika katika bruda.

v  Wiki ya  kwanza ni 35o c, wiki ya pili ni 33o c, wiki ya tatu ni 31o c na wiki ya nne  ni 29o c,
v  Kuchunguza mtawanyiko wa vifaranga ndani ya bruda ili kutathimini hali ya joto.Wakijikusanya kwenye chanzo cha joto, inaashiria kuwa baridi imezidi hivyo joto liongezwe. Wakiwa mbali na chanzo cha joto maana yake joto limezidi hivyo joto lipunguzwe,
v  Bruda iwe na sakafu yenye malalo yatokanayo na maranda ya mbao au pumba za mpunga. Malalo yabadilishwe endapo yataonekana yameloana,

v  Bruda iwekwe vifaa vya maji na chakula. Maji na chakula kiwekwe kabla ya kuweka vifaranga,
v  Vifaa vya joto viwekwe ndani ya bruda masaa 6 kabla ya kuingiza vifaranga,
v  Vifaranga walishwe chakula cha kuanzia gramu 12-15 kwa kipindi cha wiki ya 2. Katika wiki ya 3 wapewe gramu 21-35 kwa kifaranga na chakula hicho kiwepo muda wote,
v  Vifaranga wapatiwe vitamin, madini na dawa za kinga (antibiotics); na
v  Vifaranga wapatiwe chanjo kulingana na maelekezo ya mtaalamu wa mifugo.Chanjo dhidi ya magonjwa muhimu kwa mfano,Marek’s (mara anapototolewa), Mdondo (siku ya 3-4 na kurudiwa baada ya siku  ya 21 na kila baada ya  miezi 3) na Gumboro (siku ya 7na kurudia tena siku ya 21).Wapatiwa dawa ya minyoo (wiki ya 8) na coccidiosis(wiki ya 3-4). Siku ya 45 wapewe chanjo ya ndui ya kuku.
Picha hapo juu kuonyesha mfano wa bruda (kitalu).

Kutunza Kuku Wanaokua (Wiki 8-18)
Utunzaji wa kundi hili unategemea mfumo unaotumika Kuku Wanaofugwa Katika Mfumo Huria
Kuku wanaofugwa katika mfumo huu wapatiwe matunzo bora yakiwemo yafuatayo;
v  Wapewe chakula cha ziada asubuhi kabla ya kutoka na wanaporudi kwenye banda. Chakula hicho kinaweza kugawanywa  mara ya 2 kwa  siku,
v  Wapatiwe maji safi na ya kutosha wakati wote
v  Wapatiwe chanjo na dawa kulingana na ushauri wa mtaalam wa mifugo. Wiki ya kumi warudie chanjo ya mdondo, wiki ya 12 kuhara (fowl cholera), wiki ya 14 ndui ya kuku,
v  Kuku Wanaofugwa Katika Mfumo Shadidi
v  Majogoo watenganishwe na mitetea katika  wiki 7 hadi 10 ili kuzuia uzaliano usio na mpangilio,
v  Wapewe chakula cha kukuzia kuanzia wiki ya 8-15 gramu 55- 60 na kuanzia wiki ya 16 gramu 65-80 kwa wanaofugwa mfumo huria na gram 120-125 kwa kuku kwa siku kwa wanaofugwa mfumo wa shadidi,
v  Kuku wa nyama wapatiwe chakula cha kuku wa nyama muda wote,
v  Wapatiwe maji safi ya kunywa  kwa muda wote kwenye vyombo safi,
v  Kuku wachunguzwe dalili zozote za ugonjwa ili waweze kupata tiba sahihi kutoka kwa mtalaamu wa mifugo,
v  Kuku wa wiki 9-20 wanahitaji nafasi ya mita za mraba 0.15 kwa kuku na wiki 21 au zaidi mita za mraba 0.25 kwa kuku, 
v  Kuwe na vyombo maalum vya kutosha kwa ajili ya chakula na maji,
v  Wafanyiwe usafi wa banda mara kwa mara ili kuzuia magonjwa yanayotokana na uchafu
v  Wakatwe midomo ili kuzuia kudonoana.
Ukubwa wa Banda
Ukubwa wa banda utategemea idadi ya kuku na aina ya kundi la kuku. Kuku wanahitaji nafasi tofauti kutegemea umri, aina na njia ya ufugaji. Eneo la mita moja ya mraba linatosha kwa vifaranga 16 wa umri wa wiki 1 – 4. Hivyo banda lenye mita za  mradi 16 linaweza  kulea vifaranga  320 hadi wiki 4. Baada ya wiki 4 eneo hili liongezwe kutegemea  aina ya kuku na njia inayotumika katika ufugaji kama maelezo yanavyo onyesha hapo chini.
Eneo Linalohitajika Kufuga Kuku Kwenye Sakafu ya Matandazo Kutegemea na Umri na Aina ya Kuku.
Umri wa Kuku   Idadi ya Kuku kwa mita 1 ya mraba Kuku wa mayai Kuku wa nyama
Siku1 hadi wiki 4                                                              


Wiki ya 5 hadi ya 8
9                        


Wiki ya 9 hadi 20
6


Wiki 21 kuendelea  3-4  -
-



Angalizo:
Mabanda yanayozungushiwa wigo kama ilivyo katika mfumo wa nusu huria, kuku mmoja huhitaji eneo la wazi lenye ukubwa wa mita za mraba Mfano, kuku 100 huhitaji eneo la mita za mraba 1000
Utunzaji wa Kuku
Ulishaji
Kuku kama mifugo mingine uhitaji chakula chenye virutubisho vyote vinavyohitajika mwilini ili kukua upesi na kuwa na na afya nzuri .  Chakula kinachofaa ni mchanganyiko wa viini lishe mbalimbali vyenye kazi tofauti mwilini. Kila kiini lishe hakina budi kiwe katika kiwango sahihi kulingana mahitaji  ya mwili wa kuku katika umri tofauti.
Kuku anahitaji chakula chenye viini lishe vifuatavyo:
Kiini lishe

Wanga
Mafuta
Protini
Vitamini
Madini (calsium
na Fosforas)

Kinapatikana katika chakula gani

Pumba,Chenga za nafaka kama
mahindi, mtama.
Mashudu yanayopatikana baada ya
kukamua mbegu za mafuta kama
alizeti, karanga n.k
Mashudu ya karanga au alizeti.Damu
iliyokaushwa ya wanyama kama
mbuzi, ng’ombe n.k. Mbegu za jamii
ya mikunde kama maharage, kunde,
soya....
Majani mabichi kama mabaki ya
mboga za majani, michicha ya porini,
majani mabichi ya mipapai, majani ya
Lusina n.k.
Unga wa dagaa,  unga wa mifupa
iliyochomwa, chokaa

Kazi yake mwilini

Kutia nguvu mwilini
Kutia nguvu na joto
mwilini
Kujenga mwili na
kukarabati mwili
Kulinda mwili. Majani
mabichi pia huwezesha
kuku kutaga mayai yenye
kiina cha njano, rangi
ambayo huwavutia walaji
wengi.
Kujenga mifupa,
kutengeneza maganda
ya mayai




Mfano wa kuandaa vyakula vya makundi tofauti ya kuku
Kwa Vifaranga
Kwa vifaranga vya tangu kutotolewa hadi miezi miwili, tengeneza mchanganyiko ufuatao. Huu ni mfano mmojawapo wa kuandaa kilo 100 za chakula cha vifaranga. Iwapo utahitaji kuandaa jumla ya kilo 50 za chakula tumia nusu ya vipimo vilivyoainishwa katika jedwali hili. Wastani wa mahitaji ya kuku wakubwa 50 kwa siku ni kilo 5. Chakula hiki ukigawe katika sehemu mbili na kuwapatia nusu asubuhi na nusu ya pili mchana.
 Vifaranga hupewa chakula kiasi wanachoweza kumaliza (hawapimiwi).
Vifaa
Dagaa (unga au vichwa vya dagaa)
Chenga za nafaka kama mahindi au mtama n.k
Mashudu
Pumba
Chokaa
Unga wa Mifupa,Madini ( Premix)
Chumvi
Mchanga
Jumla
Kiasi kwa kilo
12 hadi 15
40
20
24
2
2
Robo kilo
1
Kilo 100

Kwa kuku wanaokua (baada ya miezi miwili ).
Vifaa
Dagaa (unga au vichwa vya dagaa)
Chenga za nafaka kama mahindi au mtama n.k
Mashudu
Pumba
Chokaa
Unga wa Mifupa,Madini ( Premix)
Chumvi
Mchanga
Jumla
Kiasi kwa kilo
7
30
20
39
2
2
Robo kilo
1
Kilo 100





Kama umeamua kufuga kuku kwa mtindo wa kuwaacha huru wajitafutie chakula (huria) unaweza kuwapatia vifaranga nyongeza ya protini.Utafanya hivyo kwa kuwachanganyia vumbi au vichwa vya dagaa kiasi cha kikombe kimoja vilivyotwangwa pamoja na pumba ya mahindi vikombe vitano.


Maji ya Kunywa
Mfugaji ahakikishe anawapatia kuku maji masafi ya kunywa na ya kutosha kila siku. Vyombo vya maji ya kunywa budi visafishwe vizuri kila siku. Hii itasaidia sana kudhibiti magonjwa yanayoweza kutokana na vimelea vya magonjwa vinavyostawi katika maji yasiyo safi. Kuku wanaweza kuwekewa maji katika aina tofauti ya vyombo kutegemea na urahisi wa kupatikana mfano sufuria, ndoo za plastik zilizokatwa kuruhusu kuku kunywa bila kuchafua.


Usafi  katika banda
Matandazo yanayowekwa katika sakafu ya banda la kuku hayana budi yageuzwe mara kwa mara kwa wastani wa kila baada ya miezi miwili au mitatu . Wakati mwingine ni kabla ya kipindi hiki muda wowote yanapoloana na maji. Matandazo uharakisha kukauka kwa unyevu katika banda unaotokana na kinyesi cha kuku na pia zaidi na maji yanayomwagika.
Usafi katika banda utasaidia kudhibiti kwa kiasi kikubwa magonjwa mbalimbali. Kuokota mayai
Usiyaache mayai ndani ya viota kwa muda mrefu, yaokote mara kwa mara ili kuepuka kuharibiwa kwa mayai hayo na kuku wenyewe. Kuku wanayo tabia ya kula mayai yao ikiwa chakula unachowapa kina upungufu wa protini.
Vilevile kiasi cha mwanga unaoingia ndani ya banda kikizidi kuku hula mayai au kudonoana wenyewe kwa wenyewe.Uonapo dalili za namna hii kwenye kundi lako punguza kiasi cha mwanga kwa kuziba sehemu za madirisha kwa vipande vya magunia au vipande vya makasha ya karatasi ngumu.
Kama ilivyoelezwa awali kuku wapewe majani mabichi ya kutosha mara kwa mara ili wawe wanakula hayo badala ya kudonoana.
Pia fuatilia kuhakikiksha kama chakula kina protini ya kutosha. Kama tatizo la kudonoana na kula mayai litaendelea omba msaada kwa mtaalam wa mifugo akuelekeze jinsi ya kuwakata au kuwachoma midomo.

Magonjwa ya Kuku

Magonjwa ya kuku yapo mengi. Hata hivyo siyo yote yanatokea mara kwa mara hapa Tanzania. IIi uweze kudhibiti yale yanayotokea katika kundi lako unahitaji kufahamu dalili za jumla za magonjwa hayo. Unapoigundua moja au zaidi ya dalili za ugonjwa au wadudu chukua hatua mara moja. Yapo magonjwa ambayo yanaweza kuangamiza kundi lote la kuku katika.muda mfupi.
Jihadhari na uwezekano wa kupatwa na hasara zinazoletwa na magonjwa ambayo unaweza kuyazuia.
Katika sehemu hii utajifunza kwa muhtasari tu dalili za jumla za magonjwa ya kuku na jinsi ya kuyadhibiti. 
Dalili za Jumla za Magonjwa ya Kuku :-
 Kuku kupoteza hamu ya kula.
 Kuzubaa na kukaa mahali pamoja kwa muda mrefu (Kutochangamka).
 Kushuka kwa kiwango cha utagaji wa mayai.
 Vifaranga kutokua upesi au kudumaa. - Macho kuwa na rangi nyekundu.
 Kujikunja shingo.
 Kutetemeka, kutoa majimaji puani, mdomoni na machoni.
 Kutoa mharo (kinyesi) wa rangi ya kijani au wenye mchanganyiko na damu au cheupe.
 Kukonda.
 Kukohoa.  
Ukion
Muhtasari wa Magonjwa Muhimu ya Kuku na Jinsi ya Kuyadhibiti na Kutibu .
a moja au zaidi ya dalili hizi katika kundi lako chukua hatua za kutibu zilizoelezwa hapa chini. Kama hali ni ngumu zaidi omba msaada kwa mtaalam wa tiba ya mifugo ili achunguze mara moja na kukushauri jambo la kufanya.
Ugonjwa.
Chanzo.
Dalili.
Kudhibiti na Kutibu.
1. Kideri
(Newcastle)
Virusi.
-Kukohoa, kupumua kwa shida.
-Mwili kukosa nguvu; -shingo kujikunja.
-Kuharisha kijani.
-Kuku hufa wengi
-Kuhara damu.
-Vifaranga wachanjwe
katika juma lao la
kwanza. Chanjo la pili
wanapofikisha umri wa
miezi 4 na nusu.
-Chanja kuku kila baada ya miezi mitatu.
2. Kuhara damu
(Coccidiosis).
Bakteria.
-Kuku hujikusanya pamoja.
-Hawachangamki.
-Hushusha mbawa.

• Tunza usafi katika
banda.
• Lisha vifaranga chakula
kilichochanganywa
na dawa ya kinga
coccidiost kama
Amprolium au Salfa.
• Watenge kuku wote
Walioambukizwa na
wapatie dawa kama
Amprolium au salfa au
Esb3.

3. Ndui ya kuku
(Fowl pox).
Virusi.
-Malengelenge kwenye,kishungi na kope za
macho na sehemu zisizo
na manyoya.
-Kuku uvimba uso na
Macho.
• Kuchanja kuku wote
wakiwa na umri wa
miezi miwili.

4. Mafua ya kuku
(Fowl coryza).
Bakteria.
-Kamasi hutirirka puani na
mdomoni
-Kuhema kwa shida hata
kukoroma.
-Kukohoa.

• Watibu wanaougua
kwa kutumia anti biotic
kama sulphamethazine,
streptomycine na
vitamin
• Usafi wa vyombo na

banda kwa ujumla
• Watenge kuku
wagonjwa

5. Kuharisha nyeupe
Bakteria.
-Kuharisha nyeupe na
hamu ya kula kupungua.
• Usafi wa vyombo na

banda kwa ujumla
• Watenge kuku
wagonjwa
• Tumia dawa kama
Furazolidone au
Sulfadimidine
• Hata vitunguu



Njia kuu za ujumla za kudhibiti magonjwa ni:
 Kutunza hali ya usa? ndani ya banda na kudhiditi kusiwe na unyevu
Matandazo yakichafuka yabadilishwe.
 Vyombo vya maji visa?shwe kila siku
Jitahidi uepuke kufuga kwa njia ya huria ili kuku wako wasiambukizwe magonjwa Kirahisi
Epuka kufuga kuku wako pamoja na bata na khanga.Hawa ni wabebaji wa vimelea vya magonjwa ya kuku japo wao hubaki


salama.




Zingatia ratiba za chanjo kwa magonja yasiyo na tiba kama kideri na mengineyo ya virusi

Kutoa chanjo ya kideri kwa njia ya kuweka matone ya dawa katika macho.

Ufugaji wa Aina Nyingine za Ndege.

Aina ya ndege wengine wanaofugwa hapa nchini ni pamoja na Bata maji, Bata bukini, Bata bukini, Kanga na Njiwa. Ndege hao hufugwa kwa kiasi kidogo ukilinganishwa na kuku kwa kuwa soko lao ni dogo.Utunzaji wao hautofautiani sana na kuku;
v  Wajengewe banda la kuishi ambalo ukubwa wake utagemea idadi ya ndege wanaofugwa,
Mambo ya kuzingatia kwa kuku wanaotaga  ni pamoja na:-  
v   Banda liwe na viota vya kutagia mayai (kiota 1 kwa kuku 3- 5).Viota viwekwe bandani mara kuku watakapofikisha  umri wa wiki 18 ili waanze kuzoea kuvitumia,
v   Wapatiwe chakula na maji safi wakati wote kwa kutumia vyombo maalum ambavyo ni visafi,
v   Kuku  wasiotaga waondolewe kwenye kundi.Kuku hao huonekana wasafi na sehemu ya kutolea yai huwa ndogo na kavu,upanga wake kichwa (comb) huwa mdogo na mwekundu,
v   Wapatiwe dawa ya minyoo kila baada ya miezi 3,
v   Wawekewe fito au ubao mwembamba kama sehemu ya kupumzikia na mazoezi ili kuzuia kudonoana,
v   Mayai yakusanywe mara 4 au zaidi kwa siku ili yasidonolewe na kuku,
v   Kuwe na malalo makavu na yabadilishwe mara yanapochafuka,
v   Vyombo vifanyiwe usafi kila ili kuzuia magonjwa; na
v   Watundikiwe majani mabichi aina ya mchicha,papai, alfaafa,majani jamii ya mikunde ili kuboresha lishe. Udhibiti na Tiba  Dhidi ya Magonjwa ya Kuku
Kuku wanaopata lishe bora, kutunzwa vizuri na kupatiwa chanjo dhidi ya magonjwa yanayotokea mara kwa mara huwa na afya nzuri. Ni bora kuzuia magonjwa kuliko kutibu ili kupunguza vifo na gharama. Iwapo ugonjwa utatokea kuku wagonjwa watenganishwe na kuku wasio wagonjwa na wapatiwe tiba. 

Kanuni muhimu za kufuata ili kuzuia magonjwa ni:-
v   Banda liwe  safi muda wote,
v  Kabla ya kuweka kuku, banda  linyunyuziwe  dawa ya kuua wadau wa magonjwa mbalimbali,

v               Wapatiwe chakula chenye virutubisho na maji ya kunywa yakutosha,

v               Wapatiwe kinga na tiba dhidi ya magonjwa,
v               Bata  maji  na  Bata  bukini  wajengewe  bwawa  lenye  nafasi  ya kukutosha kwa ajili ya kuogelea; na
v               Njiwa  wajengewe  viota  sehemu  ya  juu  kama  kwenye  mapaa  ya nyumba.

Utunzaji wa Kumbukumbu.

Utunzaji wa kumbukumbu ni muhimu sana katika ufugaji wa kuku na ndege  wengine  wafugwao  ili  kusaidia  mfugaji  kujua  maendeleo  ya ufugaji wake. Utaratibu wa kuweka kumbukumbu mara tukio linapotokea ni lazima ili kuepuka kusahau.Mfugaji ahakikishe anaweka kumbukumbu ambazo ni sahihi na zinazoeleweka.

Aina za Kumbukumbu
Kumbukumbu zinazopaswa kuwekwa ni pamoja na:-
*       Aina  na  idadi  ya  kuku  waliopo  kwenye  kila  kundi  (mfano vifaranga,wanaokua,wanaotaga,majogoo),
*       Uzalishaji wa mayai kwa kundi la kuku waliopo,
*       Utotoaji wa vifaranga,
*       Kinga na matibabu,
*       Mapato na matumizi,
*       Utagaji wa kila kuku na utunzaji (kwa kuku wa asili); na
 Kumbukumbu za vifo

No comments:

Post a Comment