JINSI
YA KUANDAA MBEGU BORA YA VIAZI MVIRINGO
Wakulima wengi wamezoea kuandaa mbegu zao za viazi
kwa kuchambua mbegu hizo mara tu baada ya kuvuna. Uchambuzi hufanyika kwa
kuangalia zile ndogondogo na kuzihifadhi kwa ajili ya msimu unaofuata. Pia kuna
wakulima wengine ambao hutegemea kupata au kununua mbegu kutoka kwa wakulima
wengine walio jirani au kwenda sehemu fulani kununua mbegu za
viazi. Hali hii
kitaalam haishauriwi, kwani kununua mbegu kwa mkulima bila kujua usalama wa
mbegu hizo, ni hatari sana, kwani hupelekea mkulima kuuziwa mbegu zenye
magonjwa au wadudu. Kwa kufanya hivyo pia huweza kuambukiza magonjwa na wadudu
kutoka shamba moja na linguine. Mkulima
anashauriwa kununua mbegu bora kutoka kwa wakulima waliosajiliwa kwa ajili ya
kuzalisha mbegu, na kuziuza kwa wakulima wa viazi vya chakula. Vile vile
mkulima anaweza kununua mbegu kutoka kwa makampuni yanayojishughulisha na
uzalishaji wa mbegu za viazi mviringo.
TEKNOLOJIA
YA KUZALISHA MBEGU ZA VIAZI MVIRINGO
Wakulima wengi hawana uwezo wa kununua mbegu za
viazi kutoka kwa makampuni yanayozalisha mbegu za viazi, kila mara. Kwa
kutambua hilo, wakulima wanashauriwa kutumia teknolojia yakuzalisha mbegu
kutoka kwenye mashamba yao ya viazi vya chakula. Zipo teknolojia za aina mbili
ambazo mkulima anashauriwa kuzitumia kwenye kuzalisha mbegu zake kwa matumizi
yake mwenyewe. Mbegu zinazozalisha kwa njia hizo, mkulima haruhusiwi kuziuza
kwani ni mbegu ambazo hazijakaguliwa na wataalam. Teknolojia hizi zinaruhusiwa
kwa wakulima wanaozalisha mbegu kwa matumizi yao binafsi.
1. TEKNOLOJIA
YA CHAGUA ILIYO BORA (Positive selection)
Hii ni teknolojia ambayo inamtaka mkulima kuchagua
mimea iliyo bora kutoka shambani kwake, kisha na kuiwekea alama na kuanza
kuihudumia vizuri kwa kuichunguza bila kuruhusu magonjwa na wadudu. Mimea hiyo
huvunwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya mbegu msimu unaofuata. Njia hii ni rahisi
na isiyokuwa na gharama, kwani mkulima hutumia mbegu zake mwenyewe na Shamba
Lake, kuandaa mbegu za viazi. Kama mkulima atafuata maelekezo ya kitaalam jinsi
ya kuchagua mimea na kuihudumia utafiti unaonesha mkulima hupata mbegu iliyo
bora sawa au karibia na sawa na mbegu zinazozalishwa na wakulima waliosajiliwa.
2. Teknolojia
ya chagua isiyo bora (Negative selection)
Hii ni teknolojia ambayo hutumiwa na wakulima hasa
wale waliotenga sehemu au shamba kwa ajili ya kuzalisha mbegu kwa matumizi yao.
Njia hii inamruhusu mkulima kuchunguza ndani ya shamba lake la mbegu, kisha
kung’oa mimea yote yenye kuonesha udhahifu wa magonjwa au wadudu. Mimea yote
inayong’olewa huteketezwa kwa kuchomwa moto, ili isiendelee kuambukiza ugonjwa
kwa mingine ndani ya shamba. Baada ya kufanya uchambuzi huo, mimea inayobaki
shambani hutunzwa vizuri hadi kufikia kuvunwa, kisha na kuhifadhiwa tayari kwa
kutumika kama mbegu msimu unaofuata.
Matumizi
ya Mbolea
Viazi mviringo ni moja kati ya mazao yanoyotumia
mbolea au virutubisho vingi shambani. Udongo huwa una aina mbalimbali za
virutubisho, ambavyo vinahitajka kwa mmea kuweza kustawi. Hata hivyo
virutubisho hivyo hupungua msimu hadi msimu kulingana na mazao yanayolimwa
shambani. Kilimo cha viazi hutumia sana virutubisho, hivyo mkulima anatakiwa
uchunguza na kujua ni aina gani ya virutubisho vimepungua kwenye udongo, ili
aweze kuongeza virutubisho kupitia mbolea za viwandani au mbolea za
asili.Mkulima anashauriwa kutumia mbolea ya asili au mbolea ya viwandani. Kama
mkulima anao uwezo wa kutumia mbolea ya asili kama Mboji, au mbolea ya wanyama
kama ng’ombe, ni vizuri kwani mbolea hii huongeza na kutunza afya ya udongo
mara itumiwapo. Mbolea ya ng’ombe mkulima anashauriwa kutumia tani 7 kwenye
hekita moja, na hii inatakiwa iwekwe kabla ya mvua kunyesha na kabla ya
kupanda. Mbolea hii hufanya kazi polepole, hivyo kutoleta matokeo kwa mmea kwa
haraka.
Mbolea za viwandani hutumika katika kilimo cha
viazi.Mbolea hii hupatikana madukani. Kwa upande wa viazi mviringo mkulima
anashauriwa kutumia mbolea ya kupandia na kukuzia ili kupata mavuno yenye tija.
Mfano wa mbolea za kupandia ni kama DAP, TSP, na NPK. Mbolea za kukuzia ni kama
CAN au wakati mwingine mkulima anaweza kutumia SA. Mbolea ya NPK yenye uwiano
wa 17:17:17, inafaa sana kwa kilimo cha viazi mvringo. Mbolea hii ni nzuri
kutokana na kwamba ina virutubisho vikubwa vitatu kwa pamoja vinavyohitajika
kwenye mmea wa viazi. Pia faida nyingine ya kutumia mbolea ya NPK ni kwamba huhitaji
kuweka tena mbolea ya kukuzia.
KILIMO
MZUNGUKO WA MAZAO
Kilimo mzunguko wa mazao ni jambo muhimu sana kwa
wakulima wa viazi, hasa wale wazalishaji wa mbegu. Kilimo mzunguko kina faida
nyingi sana kwa mkulima wa viazi. Kwa kawaida wakati wa kuvuna mkulima hawezi
kumaliza viazi vyote shambani, hali huchangia hata kuwa na magonjwa na wadudu shambani, iwapo viazi vilivyo bakia
shambani vitakuwa na magonjwa na wadudu. Ili kupunguza maambukizi, mkulima
anashauriwa kuhakikisha mabaki yote yanatolewa. Njia nzuri ya kufanya ni kuwa
na mzunguko wa mazao., kwani hii itasaidia kuondoa mabaki ya viazi hasa kipindi
cha palizi la zao husika. Kilimo mzunguko kina faida kama; kuepuka kuongezeka
kwa magonjwa na wadudu wanaopendelea kuishi na kula kwenye zao la viazi,
husaidia kuongeza rutuba ndani ya shamba, na pia mkulima hupata zao linguine la
kumletea chakula au pesa za kujikimu hasa kipindi cha msimu usiokuwa wa viazi.
MAMBO
YA KUFANYA KABLA, WAKATI NA BAADA YA KUVUNA VIAZI
Viazi vinachukua muda wa siku 90 mpaka 120 kukomaa,
tangu kupandwa. Mkulima anashauriwa kufahamu ni muda gani anatakiwa kufanya
maandalizi ya kuvuna. Kuna mambo ambayo mkulima anapaswa kufanyakama maandalizi
ya kuvuna. Mambo hayo ni kama; kukata mashina ya viazi mara ifikapo siku ya 80
mpaka 85 kabla ya kuvunwa. Kufanya hivyo husaidia kukomaa kwa ngozi ya viazi
ili vinapovunwa visipate michubuko inayoweza kusaidia kuingiza maginjwa na
wadudu ndania ya mbegu. Pia kukata kwa
mashina husaidia viazi vya mbegu kuwa na ukubwa sawa au karibia na sawa, hii ni
muhimu kwa wazalishaji wa mbegu.
WAKATI
WA KUVUNA
Zoezi la kuvuna viazi mviringo ni hatua ya mwisho ya
kuondoa viazi kutoka shambani. Wakulima wengi hutumia jembe la mkono wakati wa
kuvuna, na wakulima wachache hutumia jembe la kukokotwa na ng’ombe. Ni wakulima
wachache sana wanaotumia mashine maalum ya kuvunia viazi. Mambo ya kuzingatia
wakati wa kuvuna viazi;
1.
Hakikisha
mashina yote yamekatwa wiki 3 kabla ya kuvuna
2.
Anza kuvuna
kipindi cha kiangazi, kisichokuwa na mvua
3.
Hakikisha
wakati wa kuvuna viazi visipate michubuko ya aina yoyote
4.
Hakikisha
viazi vilivyovunwa havina unyevunyevu kabla ya kuvihifadhi kwenye ghala
5.
Chambua viazi
vyote vilivyo katika kabla ya kupeleka ghalani
6.
Hakikisha
ghala lako ni safi na limepuliziwa dawa za kuulia wadudu
7.
Weka viazi
vyako kwenye kichanja ndani ya ghala.
JINSI
YA KUHIFADHI VIAZI MVIRINGO
Viazi mviringo kama ilivyo kwa mazao
mengine, huhitaji kuhifadhiwa mara tu baada ya kuvunwa. Lakini kwa upande wa
viazi mvringo, jinsi ya kuhifadhi ni tofauti na mazao mengine. Viazi vinapovuna
huwa kwenye hali ya uhai, na hali hiyo inatakiwa kutunzwa mpaka wakati wa
kupanda kwa upande wa mbegu. Kutokana na asili ya viazi mviringo, mkulima
anashauriwa kuwa na sehemu maalum au gahala nzuri la kuhifadhia mbegu za viazi
mviringo.
SIFA
ZA GHALA LA VIAZI MVIRINGO
1.
Liwe na linaloruhusu mwanga na hewa
2.
Liwe na neti inayozuia wadudu kuingia na
kuharibu mbegu
3.
Liwe limewekewa vichanja kwa ajili ya
kuwekea mbegu
4.
Liwe limeezekwa vizuri ili kuzuia maji
ya mvua kuingia
5.
Liwe na mlango mpana wa kuweza kupitisha
gunia la mbegu au troli kupita.
nini maana ya kilimo mzunguko?
ReplyDeleteKilimo mzunguko ni kilimo cha kubadirisha mazao mwaka kwa mwaka mfano mwaka huu umelima viazi mviringo mwakani unalima hata mahindi iko hivyo
DeleteNi sahihi kuanika viazi juani vilivyochambuliwa kwa ajili ya mbegu kabla kuhifadhi ghalan?
ReplyDeleteCool and I have a super provide: Who Repairs House Siding split level house exterior remodel
ReplyDelete