Monday, 13 March 2017

KILIMO CHA VIAZI MVIRINGO

UTANGULIZI:
Viazi mviringi ni zao muhimu la chakula. Tanzania viazi mvringo husitawi zaidi katika sehemu za miinuko ambazo zina mvua nyingi na baridi kali.
UMUHIMU WA VIAZI MVIRINGO/MATUMIZI:
Viazi mviringo vina asilimia kubwa ya chakula chenye asili ya wanga. Viini kama vile vya protini, madini, vitamini na maji. Hivi vyote hutosheleza mahitaji ya mwili wa binadamu. Pia viazi mviringo hutumika kama zao la biashara kuweza kumpatia mkulima ffedhaza kujikimu na mahitaji mengineyo katika familia.Ili mkulima aweze kulima na kuzalisha kwa tija mbegu bora na kupata mavuno mengi, ni lazima afuate kanuni bora za uzalishaji wa zao la viazi.
Mambo ambayo mkulima anatakiwa kufahami ni pamoja na:
ü  Hali ya hewa kwa zao la viazi
ü  Hali na aina ya udongo
ü  Virutubisho ndani ya udongo
ü  Magonjwa na wadudu
ü  Namna ya kuvuna na kuhifadhi mbegu na viazi vya chakula.
ü  Ujenzi wa maghala ya kuhifadhia mbegu na viazi vya chakula.
Kijitabu hiki kinaelezea kanuni bora za uzalishaji wa zao la viazi mviringo. Mkulima anashauriwa kukisoma kwa makini, ili aweze kujua kwa undani hasa kwa wakulima wanao jianda kuingia katika biashara ya uzalishaji wa mbegu za viazi mviringo.

KANUNI ZA UZALISHAJI BORA WA MBEGU NA VIAZI VYA CHAKULA
1.      Uchaguzi wa shamba
Kwa ajili ya uzalishaji bora na wenye tija, lazima mkulima afahamu mambo mbalimbali yahusuyo kanuni za kilimo bora. Mija ya mambo muhimi ni uwezo wa mkulima kuweza kuchagua eneo zuri la kulima viazi mviringo, liwe kwa ajili ya mbegu au viazi vya chakula. Kuna utofauti wa eneo la viazi vya chakula na viazi vya mbegu.
Kwa ujumla viazi mviringo huhitaji mwanga wa jua wa kutosha, Udongo wenye rutuba, na usiokuwa na tindikali nyingi. Pia udongo unatakiwa ule usio twamisha maji, udongo laini, kwani udongo ukiwa mgumu, hali hii husababisha viazi kuwa na mwonekano wa tofauti au kutokuwa na ukubwa unaotakiwa.

Wakati wa kuchagua mashamba kwa ajili ya uzalishaji viazi, mkulima anashauriwa kuangalia yafuatayo;-

v  Shamba lisiwe kwenye mteremko mkali, hii ni kwasababu wakati wa kuvuna inakuwa kazi kubeba viazi kutoka bondeni, na hata hivyo wakati wa mvua nyingi maji yanaweza kuharibu mazao na kuondoa virutubisho.
v  Historia ya shamba- Ni vizuri kabla ya mkulima wa mbegu za viazi hajapanda, ajue taarifa za shamba hilo, hasa aina ya mazao yaliyopandwa msimu uliopita na historia ya magonjwa. Kwa ujumla shamba linatakiwa lisiwe na historia ya magonjwa kama ya Mnyauko bacteria, virusi, au kuwa na wadudu kama minyoo fundo au wadudu nondo wa viazi. Hali hii itasababisha mbegu kukosa ubora na hata kupunguza mavuno kwa mkulima.

Mahitaji ya viazi mviringo
Ili viazi ziweze kumea na kustawi, vinahitaji mazingira na hali ya hewa nzuri inayoruhusu viazi kustawi. Kimsingi viazi zinahitaji hali ya ubaridi na miinuko ya kuanzia erefu wa mita 800 mpaka 3000 kutoka usawa wa bahari. Hata hivyo kwa wakulima wa mbegu, wanatakiwa kuwa na mashamba ya mbegu sehemu zenye miinuko ya juu, ili kuepuka na milipuko ya magonjwa yanayo weza kushambulia na kuharibu mbegu za viazi. Viazi vinahitaji joto la wastani kuanzia 10-220C. Pia viazi vinahitaji angalau masaa 12 ya mwanga ili viweze kustawi vizuri shambani na kuleta mavuno yenye tija. Udongo unaofaa unatakiwa uwe wenye tindikali ndogo kuanzia 5.0-5.5, hivyo mkulima anashauriwa kufanya uchunguzi wa hali ya tindikali ya udongo kabla ya kupanda. Tindikali ya udongo ikizidi kiwango cha kitaalam, husababisha mazao kushindwa kupata virutubisho kutoka kwenye udongo.

Jinsi ya kutayarisha shamba
Kwa mkulima yeyote, zoezi hili ni la kawaida sana. Ili kupata mavuno yenye tija, mkulima hana budi kujua jinsi gani atayarishe shamba lake, tayari kwa kupanda viazi. Shamba la kupanda viazi linahitaji kulimwa kwa makini na kuhakikisha udongo umekuwa laini wenye kuruhusu viazi kuota kwa urahisi. Kwa wakulima wenye uwezo wanaweza kutumia trekta au jembe la kukokotwa na ng’ombe. Wakulima walio wengi wanatumia majembe ya mkono, hivyo anatakiwa kuhakikisha jembe lake linaingia chini sana ili kuweza kulainisha udongo.
Wakati wakuandaa shamba ndiyo muda mzuri wa kuondoa matakataka yote ili shamba libaki safi na salama kwa ajili ya kupanda mbegu za viazi. Faida za kutifua udongo vizuri kabla ya kupanda ni pamoja na kuongeza rutuba ya udongo, kupunguza uotaji wa magugu. Husaidia kuweka juu ya udongo vimelea vya magonjwa na wadudu hali inayosababisha wapigwe na jua kisha kufa.

Jinsi ya Kupanda
Muda mzuri kwa mkulima kupanda mbegu za viazi ni mara tu mvua za mwanzo zinapoanza kunyesha, na hali ya unyevunyevu kuwa ya kutosha kwenye udongo. Vile vile ni jambo la msingi kupanda kwa kuangalia majira, ili mimea isije ikakumbana na hali ya hewa inayoruhusu kustawi kwa mimea, mfano kipindi chenye baridi sana au joto sana au ukame, pia kuwepo na magonjwa na wadudu wasumbufu wa viazi. Hivyo mkulima anashauriwa kujua majira mazuri ya kuweza kupanda viazi. Kipindi kibaya kwa mazao ya viazi ni hatua ya mimea ya viazi inapokaribia kuchanua, hiki kipindi, mimea ya viazi haihitaji mvua nyingi, au hali ya ukame. Mkulima anashauriwa kupanda kwa matuta mara tu baada ya kufukia mbegu ardhini. Matuta yana faidi nyingi sana, kwanza yanazuia mbolea iliyowekwa isipotelee au kubebwa na maji pindi mvua inaponyesha, yanapunguza uotaji wa magugu shambani, yanarahisisha wakati wa palizi, yanasaidia kutunza unyevuunyevu, na pia yanapunguza wadudu nondo kuingia ndani ya viazi.

Nafasi ya kupanda
Kwa kawaida ili mkulima aweze kupata mavuno mengi, ni lazima azingatie nafasi ya upandaji. Kwa upande wa viazi kuna nafasi za aina mbalimbali kutegemea na lengo la mkulima pamija na aina ya mbegu za viazi. Kuna nafasi kwa ajili ya kulima viazi vya chakula na nafasi ya kupanda kwa ajili ya wakulima wanao lima mbegu za viazi. Nafasi ya kupanda ina mchango mkubwa kwenye mavuno ya viazi, hasa ukubwa wa kiazi chenyewe. Nafasi ya kupanda iliyoshauliwa kwa wakulima wa viazi vya chakula ni sentimita 75 au 80 mstari hadi mstari na sentimita 30 kiazi hadi kiazi. Nafasi hii huruhusu ukuaji mzuri na kuwa na saizi nzuri ya viazi kwa ajili ya chakula. Pia nafasi hii mkulima anatakiwa kuwa na mbegu za viazi zisizopungua 44,440 au 41,140 kwa hekta. Nafasi kwa ajili ya uzalishaji wa mbegu za viazi hutofautiana na nafasi ya uzalishaji wa viazi vya chakula. Kwa upande wa viazi vya mbegu nafasi ya kupanda ni Kati ya mmea na mmea ni sm 25 au sm 30 na Kati ya mstari na mstari ni sm 70. Hii husaidia kutengeneza viazi vyenye ukubwa mdogo ukilinganisha na viazi vya chakula. Mkulima anatakiwa kuzingatia nafasi hizi ili mbegu itakayozalishwa iwe na ukubwa unaofaa kwa mbegu. Mkulima atahitaji kiasi cha mbegu kati ya 57,140 au 47,620kwa hekta.
AINA NA UKUBWA WA MBEGU
Hili jambo la muhimu sana kwa mkulima kutambua ni aina gani ya mbegu anatakiwa kupanda na ina patikana wapi. Pia ni muhimu kujua hata ni ukubwa gani wa mbegu za viazi unafaa kutumika kupanda. Wakulima baadhi hupanda mbegu za viazi zilizo katwa vipande vipande, na wengine hutumia kiazi kizima lakini vidongo. Kitaalam inashauri mbegu ya viazi iliyosahihi kwa kupandwa haitakiwi kukatwa vipande vipande, hali hii husababisha mwanya wa wadudu na magonjwa kuingia na kushambulia mbegu mara baada ya kupanda.  Mbegu inatakiwa kuwa nzima, na yenye ukubwa wa saizi ya yai la kuku (28-35milimita).
SIFA ZA MBEGU BORA ZA VIAZI MVIRINGO
Mbegu bora ya viazi mviringo inatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:-
1.      Aina inayotambulika na isiyochanganyika na aina yoyote
2.      Isiyokuwa na magonjwa au wadudu wa aina yoyote
3.      Iwe imepitia hatua zote za kuwa mbegu
4.      Isiwe na michubuko au kidonda
5.      Iwe na ukubwa unaokubalika

6.      Iwe imechipua na kuwa na machipukizi yenye afya
IITAENDELEA,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

No comments:

Post a Comment