WADUDU WAHARIBIFU NA MAGONJWA YANAYOSUMBUA ZAO LA MAHINDI NA NJIA
ZA KUDHIBITI
A) VIWAVI JESHI Ni wadudu
aina ya funza ambao hutokana na Nondo.Hushambulia mahindi kwa kula majaniyake
pamoja na shina. Wadudu hawa huangamizwa/kudhibitiwa kwa njia zifuatazo;-
- Kuondoa vichaka karibu na shamba
- Kunyunyizia sumu za asili kama
vile Mwarobaini majuma mawili ya mwanzo.
- Kunyunyizia sumu za viwandani
endapo wadudu wameanza kuonekana km vile Karate 1ml/1l
B) FUNZA WA MABUA (MAIZE STALK BORER).
- Funza wa mabua hutoboa shina la
mahindi na kusababisha kudumaa kwa mahindi.
- Matundu, ungaunga kama wa msumeno
huonekana kwenye majani yaliyoathiriwa.
- Mashambulizi huanza juma la pili
hadi la tatu baada ya mahindi kuota.
NJIA ZA KUDHIBITI ZINAZOTUMIKA
- Kuchanganya mahindi na mazao jamii
ya mikunde km vile maharagwe
- Kung’oa mahindi yaliyoshambuliwa
- Sumu za asili mwarobaini
- Sumu za viwandani km vile Karate
C)MAIZE STREAK DISEASE (VIRUS)
Dalili za ugonjwa huu huanza kuonekana kwa jani la mhindi kuwa na
rangi nyeupe-njano.jinsi mhindi unavozidi kukua ndivyo dalili zake huonekana
zaidi, gonjwa hili pia huashilia ukosefu wa madini chuma katika mmea
· Tumia mbegu zinazostahimili gonjwa hili kama vileTMV-1, KILIMA ST,
KATUMANI ST na STAHA
· Panda mapema mahindi kwani gonjwa hili linashambulia sana wakati
ikitokea umechelewa kupana
· Tumia dawa za viwandani endapo tatizo hili litakua sugu
D). LEAF RUST
Kuna aina mbili za gonjwa hili la leaf rust.ambazo ni common leaf
rust na polysora rust
Common leaf rust
Gonjwa hili hutokea pale mmea unapoanza kutoa ua la
uchavushaji,,,hutambulika kwa kuonekana kama unga unga katika jani, na eneo
lililoathiliwa na gonjwa hili huwa na rangi ya kahawia katika hatua za mwanzo
na baadae hubadilika kuwa jeusi pale mmea unavokomaa na kusababisha mmea
kuzorota au kufa kabisa.
Polysora leaf
Hasa hasa hupatikana katika maeneo yenye uwanda wa chini,eneo
lenye unyevu unyevu hapa Tanzania.
· Panda mapema ili kuzuia gonjwa hili
· Badilisha badilisha mazao(msimu huu ukipanda mahindi katika eneo
hilo msimu ujao panda maharagwe au zao lolote lenye jamii ya mikunde ili
kuongeza rutuba)
UWEKAJI MBOLEA KATIKA MAHINDI
MATUMIZI YA MBOLEA
Mahindi hustawi zaidi yakiwekwa mbolea, iwapo mambo mengine
yanayosaidia katika kukua pia yapo kwa kiwango kinachostahili. Mbolea
inayotumiwa na wakulima wadogo mara yingi huwa haitoshi. Mahindi ya kiwango cha
juu yaweza tu kufikia kiwango cha juu cha Uzalishaji iwapo yatapewa lishe na
madini ya kutosha. Mahindi ya tani 2 kwa hekta na tani 5 kwa hekta hutumia
karibu kilo 60 N, kilo 10 za P205 na kilo 70 K20 kutoka katika udongo. Mahindi
hunyonya Nitrogen pole pole katika miezi ya kwanza baada ya kupanda, lakini
huongezeka hadi kiwango cha juu kabisa wakati wa kutoa maua na kukuza tunda
(gunzi). Mahindi huhitaji nitrogen kwa kiwango cha juu na ukosefu huwa ndio
kizingiti. Kiwango cha juu cha nitrogen kinahitajika mara tatu; kwanza wakati
wa kupanda, pili, wakati ambapo mmea umefikia sentimita 50 za urefu na tatu,
wakati matunda ya mahindi yanaanza kutoa zile nyuzi nyuzi nyororo
(silking).Udongo mwingi huwa na madini ya phosphorous (P205) na potassium (K20)
lakini sio kiwango kinachotosheleza mahitaji haswa ya mbegu za mahindi
zinapochipua. Nyunyuzia P205 karibu na mbegu ili ziote kwa haraka. K20 hutumika
kwa kiwango kikubwa lakini hitaji la mimea hubainika baada ya upimaji wa hali
ya udongo kujua kiasi cha mahitaji (soil test).Mbolea ambazo zina chumvi
chumvi na zenye kuyeyuka haraka kwenye maji huleta madhara yafuatayo:
· Huzuia viumbehai kukua hivyo kuharibu udongo.
· Hulazimisha mimea kutumia hizi chumvi chumvi hata kama mimea
haizihitaji.
· Mimea inapotumia hizi chumvi chumvi kwa kulazimishwa ukuaji wake
huvurugika na kusababisha upungufu wa afya na kinga hivyo kufanya mimea iweze
kuathiriwa na magonjwa pamoja na wadudu.
Inashauriwa kutumia mbolea ambazo ni endelevu/hai na haziyeyuki
haraka kwenye maji kwa mfano samadi, mboji na mabaki ya mimea ambazo ni nzuri
kwa udongo, mimea, mazingira, afya na faida zake ni za muda mrefu. Kama
ukitumia samadi au mboji, inashauriwa kuchanganya mbolea hizi katika udongo
kabla ya kupanda mahindi ili kusaidia kurutubisha ardhi na kuupa mmea chakula
na nguvu, baada ya mimea kuota inatakiwa kuendelea kuweka mbolea hizi mara kwa
mara. Pia mbolea hai/endelevu husaidia kuhifadhi unyevu nyevu na kupunguza ukaukaji
wa udongo. Madini ya nitrogen, phosphorous na potassium hupatikana kwenye
mbolea hai kama vile samadi, mboji, mimea mibichi yenye uwezo wa kutengeneza
nitrogen, mkojo wa mnyama na majivu. Inashauriwa kuhakikisha kuwa udongo wako
unapitisha hewa ya kutosha ili kusaidia viumbehai waishio kwenye udongo
wanaozalisha hivi virutubisho kuweza kukua.
MBOLEA ZA KUKUZIA
Ni mbolea zinazotumika baada ya mimea kuota kwa lengo la kuikuza
mimea ili itoe mavuno bora. Mara nyingi mbolea hizi zinatoa kirutubisho cha naitrojeni.
Mbolea maarufu za kukuzia katika soko la Tanzania ni kama:
Aina
za mbolea
|
|
|
Urea
|
46%
|
|
Calcium
Ammonium Nitrate (CAN)
|
23%
|
|
Sulphate
of Ammonia (SA)
|
21%
|
DALILI ZA UPUNGUFU WA MBOLEA
Ukosefu wa K20 husababisha ncha za majani kuwa na rangi ya njano
na kuunda gunzi (cob)lisilo na punje hadi juu. Ukosefu wa P205 hufanya matawi
kuwa na rangi ya samawati na mbegu zisizo laini. Dalili za ukosefu wa nitrogen
ni majani ya rangi ya manjano na mimea dhaifu mifupi. Phosphate haifyonzwi
haraka na mahindi na pia udongo mwingi wa nchi za joto hukosa madini hayo ya
phosphate. Inashauriwa unyunyuzie mbolea ya kiasili kama samadi kabla ya
kulimaili uboreshe hali ya udongo na kuongezea madini. Katika ukulima wa
kiasili, (organic farming, Nitrogen (N) hutiwa kwenye udongo kupitia kwa
upandaji wa mimea ya jamii ya mikunde (legumes) ambayo hutoa nitrogen katika
hewa, Hata hivyo mapendekezo ya kimbolea yaliyo katika misingi ya uchunguzi wa
udongo hutoa nafasi nzuri ya kupata kiasi kizuri cha mbolea bila kuweka kiwango
cha chini au juu. Omba msaada kutoka kwa mafisa ugani wa kilimo waliyo katika
eneo lako. Katika maeneo yanayo tegemea mvua kukuza mahindi, panda mbegu
wakati wa mvua ya kwanza. Hii itaruhusu mizizi kunyonya madini yaliyotengenzwa
na bakteria katika udongo. Maji yaliyosimama huyeyusha na kuondoa madini ya
nitrogen kutoka katika udongo na kusababisha ukosefu wa Nitrogen
MANUFAA YA MATUMIZI YA MBOLEA
i). Kuongeza mavuno
ii). Ubora wa mazao
iii). Kuhifadhi rutuba ya udongo
iv). Kuongeza kipato kutokana na mavuno mengi na bora
MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA
Ni muhimu kutumia mbolea za viwandani katika kilimo cha mahindi
ili kumuwezesha mkulima kupata mavuno mengi. Lakini ikumbukwe kwamba matumizi
ya mbolea ni lazima yaambatane na matumizi ya mbinu nyingine bora za kuzalisha
mahindi, kama vile:
>Kuandaa shamba
>Matumizi ya mbegu bora
>Kupalilia
>Kupiga madawa ya kuzuia na kuua wadudu na magonjwa
>Kuvuna kwa wakati unaostahili
>Kuhifadhi vizuri mahindi
Kwa maelezo zaidi, muone au wasiliana na:
1. Bwana/bibi
shamba wako.
2. Muuza
pembejeo aliye karibu nawe.
3. Kitivo
chochote cha Kilimo, vyuo vikuu vya Kilimo, na taasisi zingine vya utafiti wa
kilimo.
KUKOMAA NA KUVUNA
Kukomaa kwa mahindi hutofautiana kutokana na aina ya mbegu
iliyotumika. Lakini mahindi mengi huwa yamekomaa baada ya miezi mitano hadi
saba. Majani ya muhindi yakianza kukauka ni ishara kuwa mahindi yamekomaa na
inashauriwa kuyavuna mara moja na kuyahifadhi vizuri ili kuzuia hasara ambazo
zitatokea kutokana na kuharibiwa na magonjwa au wadudu shambani kama
yakicheleweshwa
UVUNAJI
Uvunaji hufanyika kwa kutumia mikono kwa mashamba madogo na mashine (combine harvester) hutumika kwa ajili ya mashamba makubwa, Zao la wastani la mahindi ulimwenguni mnamo mwaka 2000 lilikuwa kilogramu 4255 kwa kila hekta. Zao la wastani nchini Marekani ilikuwa kilo 8600 kila hekta, huku mataifa yaliyo chini ya jangwa la Sahara la Afrika yakivuna kilo 1316 kwa kila hekta ya shamba. Zao la wastani katika taifa la Tanzania kati ya mwaka 2001-2005 lilikuwa kati ya gunia 15-19 kwa hekta (sawa na kilo 1350-1750) Ukilima kwa kuzingatia
Uvunaji hufanyika kwa kutumia mikono kwa mashamba madogo na mashine (combine harvester) hutumika kwa ajili ya mashamba makubwa, Zao la wastani la mahindi ulimwenguni mnamo mwaka 2000 lilikuwa kilogramu 4255 kwa kila hekta. Zao la wastani nchini Marekani ilikuwa kilo 8600 kila hekta, huku mataifa yaliyo chini ya jangwa la Sahara la Afrika yakivuna kilo 1316 kwa kila hekta ya shamba. Zao la wastani katika taifa la Tanzania kati ya mwaka 2001-2005 lilikuwa kati ya gunia 15-19 kwa hekta (sawa na kilo 1350-1750) Ukilima kwa kuzingatia
ukulima wa kisasa na kanuni zake kwa Tanzania utavuna kilo 5000
kwa hecta (ukanda wa pwani) na kilo 7500 kwa nyanda za juu kama Iringa, Mbeya,
Ruvuma, Arusha n.k
Kupukusua mahindi kwa kutumia mashine ya mkono
3. UHIFADHI WA MAHINDI
Mahindi huifadhiwa ghalani baada ya kuwekwa viatilifu vya kuzuia
bungua wa mahindi Njia za kisasa za uhifadhi hutumiwa kama vile matumiz ya
ACTELLIC SUPER DUST katika uwiano wa 1kg kwa gunia 5-10 za ujazo wa 100kg.
Kiatilifu kingine ni actellic solution katika rate ya 5mls katika gunia moja la
kg 100. Njia nyingine ya kienyeji katika kuhifadhi mahindi ni kuweka juu ya
ghala ambalo chini yake kuna jiko la kupikia ambalo hutoa moshi unaotumika
kufukuza na kuua wadudu.
SOKO LA MAHINDI
Tanzania pamoja na nchi mbalimbali hapa duniani zinategemea zao la
mahindi kama chakula, Hivyo katika hali kama hii tunaona kuwa ni jinsi gani zao
hili la mahindi liliyvokua na umuhimu.katika hali ya kawaida,endapo mkulima
atajikita katika ustawishaji wa zao hili ni lazima afaidike kwani mazao yake
yatanunuliwa kwa urahisi na haraka endapo yatawekwa sokoni.
Katika maeneo tofauti tofauti hapa Tanzania, bei za mahindi
zimekuwa tofauti tofauti lakini bei elekezi ya uuzaji wa mahindi kwa gunia ni
TSH50,000 lakini bei hii imekua ikiteteleka kwa sababu ya vikwazo mbalimbali
kama vile miundombinu mibovu ya barabara na magari au usafirishaji kwa ujumla
ambavyo vinapelekea wakati mwingine bei kupanda na kushuka.
No comments:
Post a Comment