Thursday, 2 March 2017

KILIMO CHA VITUNGU SAUMU.

Contents

asia ya kati na kimekuwa kikilimwa kwa karne nyingi katika nchi za mediteranian na uingereza kuanzia karne ya nne hadi ya 16. Nchini china kitunguu saumu kilijulikana miaka 3000 iliyopita kabla ya Kristo. Kwa sasa kitunguu saumu kinalimwa India, Philippine, Brazil,Mexico, na baadhi ya nchi za kiafrika ikiwemo Tanzania.

FAIDA ZA KITUNGUU SAUMU.

Kitunguu saumu kina manufaa makubwa katika mwili wa binadamu, kiasi kwamba ni rafiki mkubwa wa moyo,mbali na kuusaidia moyo usikumbwe na maradhi, kitunguu saumu pia kinazuia saratani , huingizwa oksijeni inapotakiwa , hupunguza shinikizo la damu na kolestrol, hupambana na septini, bacteria, kuganda damu na ute. Kiungo hicho cha chakula huhami mwili  dhidi ya utitiri wa vimelea na bacteria, fangasi na maambukizi ya virusi vingine. Pia huimarisha mishipa ya moyo na damu na husaidia kuzuia shambulizi la ugonjwa wa saratani. Kitunguu saumu ni moja ya viungo asilia vinavyotia msukumo zaidi wakati wa uzalishaji wa chembechembe nyeupe za damu.

Aina za vitunguu saumu maarufu kwa matumizi ya kawaida ni tatu,

1. SOFT NECK (ngozi nyororo) - ni nyeupe huzaa kwa muda mfupi.
2. SILVER SKIN(ngozi ya fedha)- vina rangi ya silver vikikaushwa vinaweza kukaa hadi mwaka mmoja.
3. ANTICHOKE - vina rangi nyekundu kwa mbali.
katika nchi yetu ya tanzania vinapatikana vitunguu swaumu ya aina tatu

 1. Kitunguu saumu chenye mafuta makali.

2. Kitunguu saumu chenye madini ya protini

3. kitunguu saumu chenye madini, protini na mafuta mepesi.
Hiki ndicho tulacho kila siku hapa kwetu na wengi hutumia kama dawa wakati hakina sifa za kuwa dawa

Udongo

Kitunguu saumu huota zaidi ukanda wa juu kuanzia mita 900 hadi 1500. Pia huota katika udongo wa aina yeyote lakini hustawi zaidi katika udongo usiotuamisha maji. Udongo huo ni lazima uwe na mbolea ya kutosha hasa ya asili.

Ikiwa udongo wako ama ardhi unayotumia kuotesha kitunguu chako haina mbolea ya kutosha basi hakikisha unaurutubisha kwa kuweka mboji ama samadi iliyoozeshwa vizuri. Pia waweza kuweka samadi mbichi iliyotoka moja kwa moja zizini katika shamba lako kisha kulilima huku ukichanganya samadi na udongo vizuri na kuliacha kwa muda wa miezi saba hadi kumi kisha kulilima tena na kuotesha vitunguu vyako.

Mbolea za viwandani kama Ammonium Sulphate, Ammonium Nitrate, DAP, Urea na nyingine zaweza kutumika kwa kiwango kitakachoshauriwa na wataalamu wa kilimo na kwa muda sahihi japo hatukushauri sana kuitumia kwani mbolea ya samadi pekee yatosha.

Hali ya hewa

Kwa nchi ya Tanzania, zao hili huoteshwa na kustawi vizuri katika kipindi ambacho joto ama ni la wastani. Iwe ni kipindi cha baridi japo si baridi sana (Nyuzi joto 18C hadi 22C).


Utayarishaji wa shamba

Hakikisha shamba lako lipo katika eneo zuri lisilotuamisha maji na lisafishe vizuri kwa kuondoa magugu yote na kisha kuyafukia kwani ni rutuba pindi yakioza. Weka mboji na kisha lilime vizuri kwa kuchanganya mbole na udongo tayari kwa kuotesha.

Utayarishaji wa mbegu

Vitunguu vinavyoota vizuri ni vile vilivyohifadhiwa sehemu nzuri isiyokuwa na unyevu, na katika eneo lenye joto la wastani. Kama utahifadhi katika sehemu yenye joto jingi na hakuna hewa ya kutosha basi ukiviotesha vitunguu hivyo vitazalisha mavuno duni na dhaifu.

Kabla ya kupeleka shambani, chukua kitunguu saumu na kuchambua kwa kutenganisha vitunguu kimoja kimoja kisha kuchagua vile vitunguu vikubwa kwa kuwa hivi ndivyo vitakavyokupatia mavuno mengi na vitunguu vyenye ubora, kisha peleka shambani tayari kwa kuotesha.


Namna ya kuotesha

Piga mashimo kama ya kuoteshea maharage. Nafasi kati ya mche na mche iwe ni sentimeta 8-12 na kati ya mstari na mstari iwe ni sentimeta 25-30 (visiwe mbalimbali kama kitunguu maji kwani vitunguu swaumu havinenepi sana na unapootesha karibu ndipo unapokuwa na kiwango kikubwa cha mavuno.

Weka kitunguu chako katika mashimo ukihakikisha kuwa mizizi inakuwa chini na shina linaangalia juu. Hakikisha vitunguu vyako haviegemei upande wowote bali vimesimama wima.
Baada ya kuweka katika mashimo, fukia kwa udongo wa kutosha na uukandamize kwa nguvu kiasi ili kuhakikisha kitunguu chako kimekaa vizuri na hakiwezi kuanguka ama kuathiriwa na kitu chochote kama kung’olewa na mvua au maji wakati wa kumwagilia. Pia kwa kufanya hivyo utakinga mazao yako kuharibiwa na wanyama kama mbwa wakati wakikatisha na hata kuingia katika shamba lako.
 Upandaji wa vitunguu saumu.

Kuchipua

Baada ya siku kumi hadi siku kumi na sita, kitunguu swaumu kitachipua na kuanza kutoa majani hadi kumi na sita. Jani la katikati ambalo litaweka mbegu, litaendelea kukua na kupita majani mengine kwa urefu (mbegu hiyo ni kitunguu na huwa ni kimoja tu, lakini utakapokiotesha baada ya kuvuna kitaota na kuzaa vitunguu vingine vingi).

Umwagiliaji

Kwa kipindi cha mvua, huna haja kabisa kumwagilia kwani maji ya mvua tayari yanatosha. Kama ni kipindi cha kiangazi hakikisha unamwagilia vitunguu vyako kila unapoona shamba limekauka. Unaweza kumwagilia mara mbili hadi tatu kwa wiki.

Usimwagilie vitunguu wakati wa mchana au jioni. Ni vizuri sana kumwagilia wakati wa asubuhi ili kuipa uwezo wa kupambana na magonjwa kwani wakati kama wa jioni utaongeza uwezo wa vitunguu kushambuliwa na barafu na hata kuoza.

Uwe na utaratibu wa kuchunguza vitunguu vyako kama vimezaliana vya kutosha hasa baada ya miezi miwili kwa kuchimba kidogo. Ukishagundua kuwa vimezaliana vizuri, usimwagilie tena bali viache na kuvipa nafasi ya kukomaa, kwani ukiendelea na umwagiliaji basi vitunguu vyako vitaoza.

Usafi wa shamba

Mara zote shamba lako linahitajika kuwa safi kwa kilimo bora. Hakikisha unafanya usafi kwa kung’oa magugu na majani yasiyohitajika ili kuondoa ushindani baina yake na vitunguu vyako ambavyo vitakuwa vikigombea rutuba, hewa na maji.
Ni muhimu sana kufanya palizi walau mara nne hadi tano kufikia mavuno.

Kama ilivyo kwa mazao mengi ya bustani, kitunguu saumu hushambuliwa na magonjwa kama ukungu, kuoza, fangas pamoja na wadudu.

Namna ya kuondokana na magonjwa hayo

Ni muhimu sana kudhibiti magonjwa haya mara tu uonapo dalili kwa kutumia viuatilifu ili kuondokana na hasara kubwa itakayotokea.

Unatakiwa pia kufanya kilimo cha mzunguko wa mazao katika shamba lako yasiyo jamii moja ya vitunguu saumu kama kuotesha mahindi, maharage ili kuondokana na magonjwa mengine ambayo yanaweza kuwa sugu.

Pia, kuepukana na umwagiliaji wa jioni na usiku pamoja na kuotesha katika maeneo yanayotuamisha maji kutasaidia kuzuia ugonjwa wa kutu kwenye majani na fangas.
Ikiwa mimea tayari imevamiwa na ugonjwa wa kutu, basi mimea yote ing’olewe na kuchomwa ili kuikinga mimea ijayo itakayooteshwa katika shamba hilo.


Kukomaa hadi kuvuna

Kitunguu saumu huchukua miezi mitatu na nusu hadi minne kukomaa. Utagundua kuwa kitunguu chako kimekomaa na kipo tayari kuvunwa mara baada ya jani lake dogo la mwisho litakapokauka. Hapo utatakiwa kuingia shambani na kuvuna. 
Namna ya kuhifadhi

Mara baada ya kuving’oa vitunguu vyako, na majani yake yakiwa bado mabichi, chukua kamba na funga mafundo ya ukubwa kiasi (Unafunga kwenye majani), kisha vining’inize juu katika eneo lenye joto la wastani (kusiwe na unyevu wala ubaridi). Vitunguu vyako vitaendelea kukauka taratibu huku vikinyonya yale maji yote yaliyopo kwenye majani yake.

Pia waweza kuvikata majani na kupunguza mizizi baada ya kung’oa kisha kuweka darini na vitaendelea kukauka taratibu.

Kama ulitumia mbolea ya samadi au mboji, waweza kuhifadhi kitunguu chako kwa muda wa miezi saba hadi nane bila kuharibika na ikiwa umetumia mbolea za viwandani basi vitunguu vyako vyaweza kuharibika baada ya miezi mitatu au minne.

Faida za kitunguu saumu kiafya

Kutokana na tafiti mbalimbali zilizofanywa na wanasayansi kama Louis Pasteur, kitunguu saumu kimegundulika kuwa na uwezo wa kutibu na kukinga magonjwa mengi yanayomsumbua binadamu kila wakati.

Imegundulika kuwa kitunguu saumu husaidia kuzuia maradhi ya saratani pamoja na malaria kutokana na kemikali ambazo hutoka baada ya kukata ama wakati wa kutafuna.

Uchunguzi umebaini kuwa kitunguu saumu huweza kupunguza athari za kemikali nyingine zisizofaa mwilini hasa zitokanazo na moshi na kuimarisha uwezo wa seli za mwili.

Mwaka 1845, mwanasayansi Pasteur aligundua kuwa kitunguu swaumu huweza kutumika kama tiba ya vidonda na huzuia donda ndugu kwa kiasi kikubwa.

Haikuishia hapo, kitunguu saumu pia hutumika kama tiba ya mafua, kuzuia magonjwa ya moyo kwa kupungua kiwango cha lijamu, kupunguza shinikizo la damu na kurekebisha kiwango cha sukari mwilini.

Mwisho

Ni mhimu sana kuzingatia maelezo wa kitaalamu na kufuata kanuni za kilimo ili kuleta tija katika sekta mhimu ya kilimo.

9 comments:

  1. Jinsi gani naweza kupata mbegu? Na mbegu ya bei gani yaweza kutosha kwa hekari moja? Na gharama hadi kuvuna niNkiasi Gani na faida ki fedha ikoje?

    ReplyDelete
  2. Hapa kuhusu miezi ya kupanda mpaka mavuno sio kweli.kwani ni michache mno kwa mkulima ninae lima huchukua miezi sita paka saba kufika kuvunwa,maelezo mengne yako sahihi yatamsaidia mkulima anaenza kulima hili zao

    ReplyDelete
    Replies
    1. Gharama ya uzalishaj inafaa niwe na kias gn

      Delete
    2. Mkuu vitunguu swaum vinastawi sana mkoa gani?

      Delete
  3. Gunia tano naweza tunzaje?

    ReplyDelete
  4. Je ni muda gani unatumika mpaka kuvuna maana nakala zingine zinasema miezi sita Hadi saba zingine zinasema miezi mitatu Hadi mitano

    ReplyDelete
  5. Nataraji kulima zao hili je? naipataje mbegu,kiasi ekali moja,makisio ya gharama je ikoje kwa mlio lima

    ReplyDelete