UTANGULIZI
Hapo awali kitungu kilikuwa ni zao lililokuwa linapatikana porini katika ukanda wa bahari ya Mediterania. Zao hili hulimwa katika nchi nyingi za magharibi, nchi za milima zilipo kaskazini mwa dunia, likwemo bara la Afrika. Vitunguu hustawi katika hali ya hewa ya jotoridi 13°C – 24°C, hali ya hewa inayofaa kwa kuotesha na kukuzia miche kwenye kitalu ni jotoridi la
20°C – 25°C. Kwa kawaida vitunguu
huhitaji kiasi cha joto nyuzi 20°C-25°C ili kuweza kustawi na kukua vizuri.
Joto zaidi ya hapo hufanya vitunguu kudumaa na kutoweza kutengeneza viazi (bulbs).Zao
la kitunguu huhitaji unyevu muda wote wa ukuaji wake. Zao hili lina mizizi
mifupi hivyo linahitaji kumwagiliwa maji mara kwa mara.. Nchini Tanzania,
vitunguu maji hulimwa kwenye mikoa ya Iringa wilaya ya Kilolo mpakani mwa mkoa
wa Morogoro na kwenye maeneo ya mto Ruaha,mkoani Arusha sehemu za Mang’ora na
Babati, Kilimanjaro, naHapo awali kitungu kilikuwa ni zao lililokuwa linapatikana porini katika ukanda wa bahari ya Mediterania. Zao hili hulimwa katika nchi nyingi za magharibi, nchi za milima zilipo kaskazini mwa dunia, likwemo bara la Afrika. Vitunguu hustawi katika hali ya hewa ya jotoridi 13°C – 24°C, hali ya hewa inayofaa kwa kuotesha na kukuzia miche kwenye kitalu ni jotoridi la
Morogoro wilayani Kilosa sehemu za Lumuma na Malolo na baadhi ya sehemu za Mkoa wa Singida.
HALI YA HEWA.
Hali ya hewa ifaayo ni ile ya ubaridi wastani. Joto linalohitajika ni kati ya
nyuzi joto 13 hadi 24°C ingawa kwa miche iliyoko kwenye kitalu joto zuri ni la
nyuzi 20 hadi 25°C. Joto la juu hufanikisha utengenezaji wa kitunguu na
ukaukaji.
AINA YA VITUNGUU MAJI
Kuna aina nyingi ya vitunguu maji. Aina hizi zinaweza kutofautishwa kulingana
na:
(i) rangi ya ganda la nje la kitunguu kilichoishavunwa;
(ii) radha (utamu au ukali) wa kitunguu chenyewe;
(iii) mahitaji ya mwanga katika uzaaji: kuna aina yenye kuhitaji siku fupi
(mwanga wa saa 10 hadi 12 kwa siku) na aina ihitajio siku ndefu (saa 13 hadi 14
za mwanga kwa siku) ili kuweza kuweka kitunguu.
Aina za vitunguu.
Aina
|
Siku za
kukomaa
|
Umbile la kitunguu
|
Rangi ya
ganda
|
Rangi ya
ndani
|
Red
Creole
|
150
|
Nusu
bapa
|
Nyekundu
|
Nyekundu
kahawia
|
Red
Bombay
|
160
|
Duara
|
Nyekundu
angavu
|
Nyekundu
kahawia
|
Texas
Grano
|
165
|
Duara
|
Njano
(kaki)
|
Nyeupe
|
Uchaguzi wa mbegu za vitunguu vya kupanda kwa ajili ya
biashara ni lazima uzingatie yafuatayo;-
mahitaji ya soko (vitunguu vyekundu
hupendwa zaidi)
musimu wa kupanda
uwezo wa kuzaa mazao mengi
uwezo wa vitunguu kuhifadhiwa kwa
muda mrefu.
Mbegu bora
·
Ubora
wa mbegu ni muhimu sana, kwani ndiyo chanzo cha mazao bora.
·
Mbegu
bora inatoamiche yenye afya na kuzaa mazao mengi na bora.
·
Mbegu za vitunguu inapoteza uoto wake
upesibaada ya kuvunwa (mwaka1).
Mbegu nzuri zina sifa zifuatazo:-
·
Uotaji
zaidi ya 80%
·
Mbegu
safi zisiyo na mchanganyhiko
·
Zimefungwa
vizuri kwenye vyombo visivyopitisha hewa na unjevu.
Hivyo mkulima anaponunua mbegu za vitunguu azingatie
yafuatayo:-
·
Chanzo
cha mbegu
·
Tarehe
ya uzalishaji
·
Tarehe
ya kuisha muda wake
·
Kifungashio
cha mbegu.
·
Inashauriwa mbegu zenye umri zaidi ya mwaka mmoja
zisipandwe kwani uwezo wa kuota huwa mdogo sana.
Mbegu bora za vitunguu zinauzwa na
makampuni binafsi kama: ALPHA Seed Co.,
Popvriend,
Rotian Seed, Kibo Seed, East African Seed Company nk. Wasambazaji wa mbegu ni pamoja
namaduka ya TFA, na maduka ya
bembejeo za kilimo katika maduka mbalimbali.
Jinsi
ya kuandaa kitalu na kuzalisha miche.
Mbegu za
vitunguu huoteshwa kwanza kwenye kitalu kilichoandaliwa vizuri takribani wiki
mbili. Vitunguu maji huoteshwa zaidi kwa
kutumia mbegu kwenye kitalu na kisha kupandikizwa shambani.Sehemu ya kitalu ni
lazimaa iwe wazi, mbali na kivuli na kiwe karibu na chanzo cha maji.
Tengeneza tuta la ukubwa wa 1m x 2m
. Urefu na idadi ya matuta hutegemea kiasi cha
mbegu. Kiasi cha mbegu kwa hekta
moja ni kilo 6 au 2 kg kwa eka.
Weka samadi iliyooza vizuri kiasi
cha debe moja au mchanganyiko wa mbolea ya TSP na
CAN (200gm) kwa uwiano wa 1:1 kwenye
tuta changanya vizuri na udongo.
Sia mbegu kwenye mistari kwa nafasi
ya 1 sm x 20 sm. Tawanya mbegu vizuri wakati
wa kusia ili miche
isisongamane.Funika mbegu na weka matandazo ya nyasi kavu juu ya tuta na
mwagilia maji. Udongounatakiwa kuwa na unyevu kiasi mpaka mbegu ziote.
Nyasi ziondolewe mara tu mbegu
zikiota (siku7-10 kutegemea hali ya hewa).
Miche itunzwe vizuri na kitalu kiwe
katika hali ya usafi.
Miche imwagiliwe maji mpaka ifikie
umri wa kupandikiza shambani (wiki 5-6)
Matatizo ya miche kitaluni ni kama
yafuatayo:-
1.Kuoza kwa mbegu, kunyauka kwa miche
kabla na baada ya kuota. Hali hii inasababishwa naugonjwa wa ukungu.
-.Dawa za ukungu kama Dithane M45 au
Ridomil MZ,nk,huweza kudhibiti ugonjwa huo kwa kuchanganya dawa na povu la sabuni
ya mcheili dawa ishike kwenye majani.
Piauangalifu uwepo wakati wa
kumwagilia maji. Mwagilia maji wakati wa asubuhi au jioni.
NB;
Epuka kumwagilia maji wakati wa jua
kali kwani unjevunjevu hewani unaongeza na kusababishavimelea vya magonjwa.
Wadudu waharibifu ni pamoja na Chawa wekunduambao
wanashambulia majani katika kitalu ,
Sota,ambaohukata
miche na kusababisha vitunguu kukauka.
-Dawa za viwandani kama Thiodan ,
Selecron au Dusrban zinazuia na kudhibitihawa wadudu.
KUPANDIKIZA VITUNGUU SHAMBANI
Baada ya wiki 5 au 6, kutegemeana na
hali ya hewa miche itakuwa tayari kupandikizwa
shambani. Miche iimarishwe kwa
kusitisha maji, wiki moja kabla ya kupandikiza.
Shamba liwe sehemu isiyokuwa na
mwinuko, sehemu ya wazi ambayo haijalimwa
vitunguu kwa muda wa miaka 2 -3.
Shamba liwe karibu na chanzo cha maji kwa ajili ya
umwagiliaji. Matuta 1m x 3m au
majaruba ya 2mx 3m.yanafaa kwa kupanda miche. Matuta au
majaruba yanarahisisha umwagiliaji,
palizi na unyunyiziaji wa dawa.
Miche hupandikizwa
inapokuwa na urefu wa sentimita 10- 15 na unene 1/2 au 3/4 ya penseli kwenye
shina. Miche hii huwa imetimiza umri kati ya wiki 7 hadi 9 kulingana na
matunzo. Miche inapandikizwa kwenye nafasi ya upana wa sentimita 20 hadi 30 na
nafasi ndani ya mstari ni sentimita 10 hadi 15.
Matumizi ya mbolea
Vitunguu maji vinamahitaji makubwa ya
rutuba ya udongo. Hukua vizuri vinapopata samadi ya kutosha kiasi cha tani 25
hadi 40 kwa hekta. Mbolea isambazwe shambani baada ya kupandikiza, lakini ni
vizuri zaidi kama ikichanganywa kwenye udongo kabla ya kupandikiza. Kwa
kuzingatia mazao ya tani 18 kwa hekta, vitunguu huchukua virutubisho kutoka kwenye
udongo, kiasi cha wastani wa kilo 66 za nitrojeni, 11 za fosiforasi na 70 za
potasiumu.Hivyo kiasi cha mbolea kinachopendekezwa ni kilo 450 hadi 565 za
mbolea ya NPK (10-10-20) kwa hekta. Mbolea huwekwa siku 7 hadi 10 kabla ya
kupandikiza. Kisha, inapendekezwa kuweka kiasi cha kilo 13 hadi 18 za Nitrojeni
baada ya wiki tatu hadi nne, ili kuongeza ukuaji wa mimea. Upungufu wa kirutubisho
cha Nitrojeni unaharakisha ukomaaji na unapunguza ukubwa wa kitunguu.
Kirutubisho hiki kikizidi kupita kiasi huongeza ukubwa wa kitunguu na unene wa
shingo ya kitunguu, tabia ambayo hupunguza ubora.
UMWAGILIAJI:
Umwagiliaji mzuri unahitajika ili kupata vitunguu bora. Umwagiliaji wa maji
yanayokwenda chini kiasi cha sentimeta moja au zaidi kwa wiki ni mzuri kwa
kupata vitunguu vikubwa. Epuka umwagiliaji kupita kiasi au pungufu kwani hali
hii huweza kusababisha mipasuko wa vitunguu.
UDHIBITI WA MAGUGU
Ukuaji na mavuno yanaathirika sana endapo magugu hayatadhibitiwa mapema. Magugu
yanadhibitiwa kwa kutumia madawa ama jembe dogo la mkono. Wakati mwingine ni
mchanganyiko wa madawa, jembe la mkono na kung’olea kwa mkono.
UDHIBITI WA MAGONJWA
1. Ukungu wa unga (powdery mildew) na
wa chini (Downy
mildew)
mildew)
Magonjwa haya
hushambulia majani ya mimea shambani na hata miche michanga. Kwenye majani
kunaonekana vidoa vyeupe hasa kwenye majani makuu ya mimea michanga. Ukungu
mweupe unatokea na kuongezeka kwa haraka kwenye sehemuza baridi au nyakati za baridi.
Viini huishi kwenye mabaki ya mimea ya vitunguu na huweza kupeperushwa mbali na
upepo. Kwenye mimea michanga ugonjwa unaweza kudhibitiwa na madawa kama
mancozeb,Dithane-M45, Ridomil, Topsin M70 na
Cupric Hydroxide (Champion).
2.
Ugonjwa wa doa la pinki (Purple blotch)
Huu nao ni ugonjwa uletwao na Ukungu
na hushambulia majani, shingo na vitunguu vilivyokomaa. Huanza kama doa dogo
linalozama ndani ya jani na kisha linaongezeka ukubwa na kufanya baka la rangi
ya Zambarau ambalo huonekana katikati ya jani ambalo baadaye huwa jeusi. Shina
lililoshambuliwa hulegea na kuanguka katika wiki ya tatu au ya nne baada ya
dalili za ugonjwa kuonekana. Vitunguu vilivyokomaa huoza kuanzia shingoni na
hugeuka rangi kuwa ya njano iliyochanganyika na nyekundu.
jinsi
ya kuzuia ugonjwa.
Zuia ugonjwa huu kwa kufanya
yafuatayo:-
- Kupanda aina ya vitunguu visivyoshambuliwazaidi na
ugonjwa huu mfano Red Creole.
- Kubadilisha mazao
- Vuna vitunguu kwa wakati sahihi
- Matumizi ya mbolea zenye kalisiamu,
fosifeti napotashiamu hupunguza kuenea kwa ugonjwa huu.
- Kwa upande mwingine,matumizi ya mbolea ya nitrojeni kwa
wingi au kwa kiasi pungufu huongeza mlipuko wa magonjwa.
- Viatilifu kama vile Mancozeb Dithane-M45,
Ridomil, Topsin M70 na Cupric Hydroxide (Champion).
3.Kuoza kwa shingo (Neckrot)
Husababishwa
na ukungu na hupendelea vile vile hali ya unyevunyevu. Hushambulia zaidi
vitunguu vilivyohifadhiwa. Ugonjwa huu husababisha vitunguu kuwa laini,
hubonyea na huonekana kama vilivyopikwa. Huanzia kwenye shingo na baadaye
huenea kwenye kitunguu chote na kufunikwa na ukungu wa kijivu.
Namna ya
kuzuia:-
- Vuna vitunguu kwa wakati
sahihi
- Kubadilisha mazao
- Tumia
njia sahihi wakati wa kuvuna, epuka kuchubua au kukikwaruza wakati wa
kuvuna
- Kausha
vitunguu vizuri baada ya kuvuna
Hali hii inaweza kutokea shambani au wakati wa hifadhi ghalani. Ugonjwa huu ni hatari zaidi kwenye sehemu za joto na zenye kutuamisha maji. Ni vyema kuhakikisha kwamba shambani hakuna hali ya kutuamisha maji na pia kwenye ghala kunakuwa na hali nzuri ya mzuunguko wa hewa.
4.Kinyausi (Damping –
off)
Ugonjwa huu unasababishwa na fangasi
na kuenezwa na udongo, mbegu na masalia ya mazao.
Ugonjwa huu unasababisha mbegu kuoza
kabla ya kuota na kunyauka kwa miche baada ya kuota.
Ugonjwa unajitokeza hasa kitaluni
ikiwa hali ya hewa ina unyevunyevu na udongo una maji
maji.
Njia za kudhibiti ni kama
zifuatazo:-
·
mbegu
ziwe safi na ziwekwe dawa ya thiram
·
kutumia
mzunguko wa mazao
·
kusia
mbegu kwa nafasi za kutosha
·
kuepukana
na kubananisha miche kitaluni
·
kuepuka
kumwagilia maji wakati wa jua kali au wakati kuna ukungu
5.Virusi njano vya vitunguu (Onion yellow Dwarf virus)
Ugonjwa huu unasababishwa na virusi
na kuenezwa na wadudu aina ya vidukari (wadudu
mafuta).
Dalili za ugonjwa ni:-
·
mistari
ya rangi ya manjano kwenye majani.
·
kujikunja
kwa majani
·
majani
kugeuka rangi ya manjano na kuanguka
·
mmea
mzima kudumaa, kujikunja na kufa.
Njia za kudhibiti ugonjwa huu ni:-
·
kutumia
mbegu safi
·
kuweka
shamba katika hali ya usafi
UDHIBITI WA WADUDU
Utitiri wa vitunguu (Onion thrips), Funza wa vitunguu (Onion maggots) na Minyoo
ya vitunguu (Onion wireworms) ni miongoni mwa wadudu wasumbufu kwenye zao la
kitunguu.
1. Utitiri wa vtunguu (Onion thrips)
Hawa ni wadudu wadogodogo sana ambao hula kwa kukwaruza juu ya jani na kunyonya
majimaji ya kwenye mmea. Hali husababisha kutoka kwa mikwaruzo myeupe kwenye
majani ya vitunguu. Mashambulizi yakizidi majani huanguka na kunyauka. Ukubwa
wa
vitunguu hupungua. Hili ni tatizo kubwa zaidi hasa wakati wa ukame kuliko wakati wa unyevu hivyo athali ni kubwa wakati wa kiangazi.
vitunguu hupungua. Hili ni tatizo kubwa zaidi hasa wakati wa ukame kuliko wakati wa unyevu hivyo athali ni kubwa wakati wa kiangazi.
2. Bungua weupe (White grub)
Huyu
ni aina ya funza mkubwa. Hutaga mayai yake kwenye uozo wa majani na samadi na
hivyo mashamba ya vitunguu yaliyoko karibu au kwenye maeneo ya jinsi hiyo huwa
kwenye hatari zaidi. Hushambulia mizizi na kusababisha kukauka kwa mimea.
Kutifulia shamba na kuwaweka wazi wadudu hawa kunapunguza idadi yao.
3.Vipekecha majani (leaf miners).
Hawa ni aina ya nzi wadogo, ambao
viwavi wake wanashambulia majani, kwa kupekecha na
kutengeneza mitandao ya mitaro
kwenye majani. Viwavi wanashambulia majani na
kusababisha majani kukauka. Upungufu
mkubwa wa mazao hutokea.
Njia ya kudhibiti:
·
kupulizia
dawa ya wadudu kama karate, Selecron na Dursban.
·
kuteketeza
masalia ya mazao.
·
kutumia
mzunguko wa mazao.
KUVUNA
NA KUHIFADHI VITUNGUU
Kabla ya kuvuna vitunguu kagua
shamba ili kuhakikisha kuwa vitunguu vimekomaa.
Dalili ya vitunguu kukomaa ni:-
·
majani
kunyauka na kuanza kukauka
·
asilimia
75 -100% kuangusha shingo na majani kukauka.
Kuvuna
Vitunguu vinavunwa kwa mikono. Mimea
inang’olewa au kuchimbuliwa kwa kutumia rato
(jembe uma). Baada ya kuvuna
vitunguu vinaweza kuachwa shambani vikiwa vimefunikwa na
majani kukinga jua kali kwa muda wa
siku mbili au tatu kutegemeana na hali ya hewa. Lengo ni
kuimarisha ngozi ya vitunguu na
kufanya michubuko na majeraha madogo madogo yanayotokea
wakati wa kuvuna kuwa magumu na
kutengeneza mokovu ambayo yanazuia vimelea vya
magonjwa kuingia ndani. Pia
kupunguza unyevu kwenye majani na mashina na kuruhusu
sehemu ya chini ya shingo kufunga.
Ikiwa usalama ni mdogo, vitunguu vinachambuliwa na
kukatwa majani na mizizi na kuanikwa
sehemu nyingine.
Kuchambua
Tenga vitunguu vilivyooza, kuchubuka
na kupasuka. Vitunguu vizuri vikaushwe peke
yake.
Iwapo vitunguu vitahifadhiwa kwa
kuning’iniza kwenye chaga, basi shingo zisikatwe, bali
zisukwe na kufungwa pamoja, na
kuning’inizwa.
Kukausha
Hatua hii ni muhimu ili kupunguza
unyevu, kufanya vitunguu viwe vigumu na kuwa katika hali
ya kulala bwete.Vitunguu vinaweza
kukaushwa kwa kuninginiza kwenye chaga zilizopangwa
mfano wa dari ndani ya banda au
kutandaza kwenye kichanja chenye kuruhusu mzunguko wa
hewa pande zote, chini ya kivuli
sehemu kavu. Epuka kukausha vitunguu chini ya aridhi
na hasa sehemu zenye jua kali. Jua
linababusha vitunguu na kusababisha uharibifu. Ukaushaji
huchukua muda wa siku 7 au zaidi
kutegemeana na hali ya hewa.
Kupanga
madaraja
Vitunguu vinachambuliwa tena baada
ya kukausha ili kuondoa vitunguu vyote vyenye ugonjwa
au dalili za ugonjwa, vilivyoota na
kutoa mizizi na vyenye shingo nene. Vitunguu vinapangwa
kwenye madaraja mbalimbali kufuata
ukubwa, umbo au rangi. Hii inawezesha kupata soko zuri
na kuepuka upotevu mkubwa wakati wa kuhifadhi.
Kufungasha
na kuweka vitambulisho.
Vifungashio vinavyopatikana ni
mifuko ya nyavu vyenye uwezo wa ujazo wa kilo 20 au
magunia ya katani. Mifuko ya nyavu
ina ujazo mdogo na pia inarahisisha ubebaji. Magunia ya
katani yanatumika lakini yanaficha vitunguu
visionekane pia vinachukua mzigo mzito na kuleta
usumbufu wakati wa kupakia na
kupakua.
Vitambulisho vinawekwa kwenye
vifungashio ili kusaidia wasafirishaji kujua mzigo ulikotoka
na pia kutangaza bidhaa inayohusika
kwenye masoko ya nje na ndani.
Kwa
soko la nje ya nchi, vitambulisho vinatakiwa kuwa na habari zifuatazo:
Jina la bidhaa mfano. Vitunguu
Mango’la Red
Uzito kamili mfano. 20 kg
Jina na anwani ya mkulima au
kikundi, jina na anwani ya msafirishaji
Jina la kijiji wilaya, Mkoa na nchi
mfano. Igurusi, Mbarali, Mbeya, Tanzania
Grade 1
Kwa soko la ndani ya nchi,vitambulisho
vinakuwakuwa na habari zifuatazo:
·
Jina la bidhaa.mfano.vitunguu
Mango,la Red
·
Uzito kamili mfano. 20 kg
·
Jina la mkulima au kikundi na anwani
mfano,HEBRON VENANCE au JITEGEMEE, Box 200, Mbarali-Mbeya
·
Jina na anwani ya msambazaji mfano:Mr.
NEBART CHALAJI Box 172, Mbarali.
Usafirishaji wa vitunguu.
Uangalifu wakati wa kupakia,
kusafirisha na kupakua ni muhimu ili kuepukana na uharibifu na
upotevu wa vitunguu. Mara nyingi
vitunguu vinaharibika kutokana na ujazo kupita kiasi kwenye
vifungashio na vyombo vya usafiri,
pia kutokana na upakiaji na mpangilio mbaya, ambao
unasababisha ugandamizaji na
kubonyea kwa vitunguu.
Wakati wa usafirishaji
yafuatayoyazingatiwe:-
·
kutumia
vyombo vya usafiri vinavyofaa hasa magari yenye nafasi ya kutosha na
yenyekupitisha hewa.
·
kupanga
mifuko katika tabaka zenye safu zisizidi tatu.
·
mifuko
isitupwe wakati wa kupakia na kupakua.
·
vitunguu
visichanganywe na mazao mengine.
KUHIFADHI
Vitunguu vinahifadhiwa kwenye
maghala bora kama kribu au mabanda ambayo yanaruhusu
hewa na paa kuezekwa kwa nyasi ili
kupunguza joto.
Utengenezaji wa kribu.
Kribu inajengwa kwa fito au mianzi
na kuinuliwa juu mita moja toka usawa wa aridhi. Upana
wa kribu uwe kati ya sm 60 na 150
ili kuruhusu upepo kupita kwa urahisi. Upepo unaondoa
unyevu na joto kwenye vitunguu.
Kribu igawanywe sehemu mbili zenye kina cha sm 60 kila
moja na kutenganishwa na uwazi was m
30, ili kuruhusu mzunguko wa hewa.
kutengeneza kribu yaafutayo yazingatiwe:-
·
Kribu
ijengwe kwenye sehemu yenye upepo
·
Kribu
iezekwe kwa nyasi ili kudhibiti joto na jua
·
Miguu
ya kribi iwekwe vizuizi vya panya.
·
Weka
vitunguu tabaka mbili na kina cha vitunguu kisizidi sm 60
·
Hifadhi
kwa kuning’iniza vitunguu kwenye banda
Hili ni banda lenye uwazi mkubwa,
lenye upana usiozidi mita tano, na urefu toka chini hadi
juu usizidi mita 2½. Banda
linajengwa kwa miti, fito, mbao au mianzi na vitunguu
vinahifadhiwa kwa kuning’iniza
kwenye fremu za fito ndani ya banda. Safu za vitunguu
hupangwa kufuata urefu wa banda na
kimo cha banda. Urefu wa banda huelekezw a kwenye
mkondo wa upepo ili kuruhusu upepo
kuingia na kutoka. Banda liezekwe kwa nyasi ili
kudhibiti joto na jua. Kribu au
banda vinahifadhi vitunguu vizuri kwa muda wa miezi sita
bila kuharibika.
Upotevu wa vitunguu ghalani.
Vitunguu vingi hupotea wakati wa
kuhifadhi kwa sababu ya:-
·
Kuoza
·
Kuota
(toa majani na mizizi)
·
Kupoteza
uzito
a) Kuoza
Kuoza kwa vitunguu vikiwa ghalani
kunasababishwa na vimeliea vya fangasi au bacteia. Joto
pamoja na unyevunyevu ndani ya
ghala, kunasababisha kuzaliana na kuongezeka kwa vimelea
vya magonjwa
Kudhibiti:
-Weka ghala katika hali ya usafi, kausha
vizuri na chambua vitunguu kabla ya
kuhifadhi.
b)
Muozo Kitako (Bottom rot or basal
rot)
Vimelea vya aina ya fangas
vinavyoishi kwenye udongo, vinashambulia sehemu ya chini ya
vitunguu. Vimelea hupenya kwenye
sehemu zenye michubuko, inayotokea wakati wa palizi,
kuvuna au kusafirishwa.
Njia zifuatazohutumika kudhibiti:-
·
mzunguko
wa mazao ghalani.
·
uchambuaji
mzuri kabla ya kuhifadhi
·
kuepuka
michubuko wakati wa palizi na kuvuna.
·
Kuwa
na kucha fupi ili kuzuia michubuko kwenye vitunguu.
c)
Ukungu mweusi (Black mould).
Ugonjwa huu unaletwa na vimelea vya
fangasi, vinavyoishi kwenye udongo. Vimelea
vinazaliana katikati ya maganda na
ukungu mweusi kama poda unaonekana. Baadaye maganda
yanasinyaa na kuvunjika.
Kudhibiti ugonjwa huu;-
·
kutumia
mzunguko wa mazao ghalani.
·
kukagua
ghala mara kwa mara na kuondoa vitunguu vilivyooza
·
kuweka
ghala katika hali ya usafi.
·
Kuondoa
masalia ya vitunguu na kuchoma moto.
d)
Kuoza shingo (Neck rot)
Vimelea vya fangasi vinashambulia
vitunguu vikiwa shambani kabla ya kuvuna. Ugonjwa
hauonekani mpaka vitunguu vikomae,
vivunwe, vikaushwe na kuhifadhiwa ghalani, ndipo
ugonjwa hujitokeza. Ugonjwa
unasababisha kuoza kwa vitunguu. Maganda ya vitunguu
yanalainika kuanzia shingoni na
nyama ya kitunguu huwa na sura ya maji maji.
Vitunguuvilivyooza hunyauka na
kusinyaa.
Kudhibiti;
·
kukausha
vitunguu vizuri kabla ya kuhifadhi
·
kuchoma
na kuharibu masalia ya vitunguu shambani na ghalani.
e)
Muozo laini (Bacterial soft rot)
Ugonjwa unasababishwa na vimelea vya
bacteria. Dalili kubwa ya ugonjwa huu ni kulainika
kwa vitunguu na kutoa harufu mbaya.
Ukiminya kitunguu, maji yenye harufu mbaya hutoka
kwenye shingo. Muozo laini unatokea
wakati hali ya hewa ikiwa na unyevunyevu na joto. Pia
vitunguu vyenye shingo nene ambavyo
havijakauka vizuri ni sehemu nzuri sana ya vimelea
kuzaliana.
Kudhibiti :
Ukaushaji wa haraka na wa uhakika
baada ya kuvuna unapunguza sana ugonjwa huu
Kuota na kupoteza uzito wa vitunguu
Vitunguu vinakuwa katika hali ya
kulala bwete bila kuota kwa zaidi ya miezi sita ikiwa hali ya
hewa ghalani ni nzuri. Unyevunyevu
mwingi ghalani ni adui mkubwa wa vitunguu
vilivyohifadhiwa kwani inasababisha
kuota kwa majani na mizizi. Pia hewa ikiwa kavu sana
vitunguu hupoteza maji upesi na
kusinyaa. Kuongezaka kwa joto na unyevunyevu ndani ya ghala
kutokana na mzunguko mbaya wa hewa,
uchafu ghalani, ukaushaji na uchambuaji mbaya
vinasababisha uharibifu mkubwa wa
vitunguu ghalani
Kudhibiti ;
·
Ghala
liwe safi pia liwe na uwezo wa kupitisha hewa kavu na ubaridi wa kutosha.
·
Ghala
lijengwe sehemu yenye upepo na kuruhusu mzunguko mzuri wa hewa.
·
Vifungashio
vya vitunguu vipangwe vizuri ili kuruhusu hewa kupita juu na chini.
·
Vitunguu
ndani ya kribu/ghala vijazwe kina cha sentimeta 30-50.
·
Vitunguu
vichambuliwe vizuri kabla ya kuhifadhi.
·
Vitunguu
ghalani vikaguliwe mara kwa mara ili kuondoa vitunguu vilivyoharibika
UUZAJI WA VITUNGUU
Watu wa aina mabalimabali wanahusika
na ununuzi na uuzaji wa vitunguu wakiwa ni pamoja na:
wakulima, wachuuzi, wafanya biashara
ndogondogo, wauzaji wa jumla, wauzaji wa rejareja, wasafirishajina madalali.
Ili koboresha uuzaji na kipato cha mkulima ni muhimu
kuzingatia yafuatayo:
·
Kuboresha
ujazo kwa kufuata vipimo vinavyokubalika (kufuta lumbesa).
·
Kupeana
habari za masoko na bei kwa kutumia mitandao ya simu, kijamii na vyombo ya
habari kama redio na magazeti.
·
Kuboresha
usafirishaji kwa kutumia vikundi.
·
Kuwepo
na mtiririko wa kuuza vitungu mwaka mzima, kwa kuboresha hifadhi ikiwa
·
Ni
pamoja na maghala.
·
Kutathimini
na kuzingatia ubora wa vitunguu.
·
Kutathimini
na kuboresha ufungashaji na usafirishaji.
No comments:
Post a Comment